Zaburi 32:1-11

  • Wenye furaha ni wale waliosamehewa

    • “Nikaungama dhambi yangu kwako” (5)

    • Mungu hukupa ufahamu (8)

Wa Daudi. Maskili.* 32  Mwenye furaha ni mtu ambaye amesamehewa kosa lake, ambaye dhambi yake imefunikwa.*+   Mwenye furaha ni mtu ambaye Yehova hamwoni kuwa mwenye hatia,+Asiye na udanganyifu katika roho yake.   Niliponyamaza, mifupa yangu ilidhoofika kwa sababu ya kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.+   Kwa maana usiku na mchana mkono wako ulinilemea.*+ Nguvu zangu zilitoweka* kama mvuke katika joto kavu la kiangazi. (Sela)   Mwishowe nikaungama dhambi yangu kwako;Sikufunika kosa langu.+ Nilisema: “Nitaungama makosa yangu kwa Yehova.”+ Nawe ukanisamehe kosa la dhambi zangu.+ (Sela)   Ndiyo sababu kila mtu aliye mshikamanifu atasali kwako+Maadamu unapatikana.+ Ndipo hata mafuriko hayatamfikia.   Wewe ni mahali pangu pa kujificha;Utanilinda nisipatwe na taabu.+ Utanizunguka kwa kelele za shangwe za ukombozi.+ (Sela)   “Nitakupa ufahamu na kukufundisha njia unayopaswa kufuata.+ Nitakupa ushauri jicho langu likikutazama.+   Usiwe kama farasi au nyumbu, asiye na uelewaji,+Ambaye ni lazima msisimko wake udhibitiwe kwa hatamu au lijamuKabla hajakukaribia.” 10  Mwovu ana maumivu mengi;Lakini mtu anayemtumaini Yehova amezungukwa na upendo Wake mshikamanifu.+ 11  Furahini kwa sababu ya Yehova na kushangilia, enyi waadilifu;Pazeni sauti kwa shangwe, ninyi nyote mlio wanyoofu moyoni.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “imesamehewa.”
Au “hasira yako ilinilemea.”
Au “Unyevunyevu wa uhai wangu ulibadilika.”