Zaburi 33:1-22

  • Sifa kwa Muumba

    • “Mwimbieni wimbo mpya” (3)

    • Yehova aumba kupitia neno lake na roho yake (6)

    • Taifa la Yehova lina furaha (12)

    • Jicho la Yehova hulinda (18)

33  Pazeni sauti kwa shangwe, enyi waadilifu, kwa sababu ya Yehova.+ Ni jambo linalofaa kwa wanyoofu kumsifu yeye.   Mshukuruni Yehova kwa kinubi;Mwimbieni sifa* kwa kinanda chenye nyuzi kumi.   Mwimbieni wimbo mpya;+Pigeni nyuzi kwa ustadi, na kupaza sauti kwa shangwe.   Kwa maana neno la Yehova limenyooka,+Na kila jambo analofanya linategemeka.   Anapenda uadilifu na haki.+ Dunia imejaa upendo mshikamanifu wa Yehova.+   Kwa neno la Yehova mbingu ziliumbwa,+Na kwa roho ya* kinywa chake kila kitu kilichomo kiliumbwa.*   Huyakusanya maji ya bahari kana kwamba ni bwawa;+Huyaweka mawimbi makubwa ya maji katika maghala.   Dunia yote na imwogope Yehova.+ Wakaaji wa nchi* na wamhofu.   Kwa maana alisema, ikawa;+Aliamuru, ikasimama imara.+ 10  Yehova amevuruga njama za* mataifa;+Ameharibu mipango* ya mataifa.+ 11  Lakini maamuzi* ya Yehova yatasimama milele;+Mawazo ya moyo wake ni ya kizazi baada ya kizazi. 12  Lenye furaha ni taifa ambalo Mungu wake ni Yehova,+Watu ambao amewachagua kuwa miliki yake mwenyewe.+ 13  Yehova anatazama chini kutoka mbinguni;Anawaona wanadamu wote.+ 14  Kutoka katika makao yake,Anawakazia macho wakaaji wa dunia. 15  Yeye ndiye anayeumba mioyo ya wote;Huchunguza kazi zao zote.+ 16  Hakuna mfalme anayeokolewa na jeshi kubwa;+Mtu hodari haokolewi na nguvu zake nyingi.+ 17  Farasi ni tumaini la uwongo la wokovu;*+Nguvu zake nyingi hazimhakikishii mtu kwamba ataponyoka. 18  Tazama! Jicho la Yehova linawalinda wale wanaomwogopa,+Wale wanaongojea upendo wake mshikamanifu, 19  Ili awaokoe* kutoka katika kifoNa kuwahifadhi hai wakati wa njaa kali.+ 20  Tunamtarajia Yehova. Yeye ni msaidizi wetu na ngao yetu.+ 21  Mioyo yetu hushangilia kwa sababu yake,Kwa maana tunalitumaini jina lake takatifu.+ 22  Upendo wako mshikamanifu na ukae juu yetu, Ee Yehova,+Tunapoendelea kukungojea.+

Maelezo ya Chini

Au “Mpigieni muziki.”
Au “pumzi ya.”
Au “jeshi lote la mbinguni liliumbwa.”
Au “ardhi inayozaa.”
Au “mawazo.”
Au “mashauri ya.”
Au “mashauri.”
Au “la ushindi.”
Au “aokoe nafsi zao.”