Zaburi 35:1-28

  • Sala ya kuomba ukombozi kutoka kwa maadui

    • Maadui watafukuzwa (5)

    • Kumsifu Mungu katikati ya umati wa watu (18)

    • Achukiwa bila sababu (19)

Wa Daudi. 35  Ee Yehova, itetee kesi yangu dhidi ya wapinzani wangu;+Pigana na wale wanaopigana nami.+   Chukua ngao yako ndogo* na ngao yako kubwa,+Inuka unitetee.+   Inua mkuki wako na shoka lako la vita* dhidi ya wale wanaonifuatia.+ Niambie:* “Mimi ni wokovu wako.”+   Wale wanaowinda uhai wangu* na waaibishwe na kufedheheshwa.+ Acha wale wanaopanga njama ya kuniangamiza wakimbie kwa aibu.   Na wawe kama makapi katika upepo;Malaika wa Yehova na awafukuze.+   Njia yao na iwe na giza na uteleziMalaika wa Yehova anapowafuatia.   Kwa maana bila sababu wameficha wavu wa kunitega;Na bila sababu wamenichimbia shimo.   Msiba na umjie kwa ghafla;Wavu aliouficha na umnase;Na aanguke ndani yake na kuangamizwa.+   Lakini mimi nitashangilia kwa sababu ya Yehova;Nitakuwa na shangwe kwa sababu ya matendo yake ya wokovu. 10  Mifupa yangu yote itasema: “Ee Yehova, ni nani aliye kama wewe? Unawaokoa wasio na uwezo kutoka kwa wale wanaowazidi nguvu,+Wasio na uwezo na maskini kutoka kwa wale wanaowanyang’anya.”+ 11  Mashahidi wenye nia mbaya hunikabili,+Na kuniuliza mambo nisiyoyajua. 12  Wananilipa uovu kwa mema niliyotenda,+Na kunifanya nihisi kama mtu aliyefiwa. 13  Lakini walipokuwa wagonjwa, nilivaa nguo za magunia;Nilijitesa kwa kufunga,Na sala yangu ilipokosa kujibiwa,* 14  Nilitembea huku na huku nikiomboleza kana kwamba ninamwombolezea rafiki au ndugu yangu;Niliinama chini kwa huzuni, kama mtu anayemwombolezea mama yake. 15  Lakini nilipojikwaa, walishangilia na kukusanyika pamoja;Walikusanyika pamoja ili wanivizie na kuniua;Walinirarua vipandevipande nao hawakunyamaza. 16  Wasiomwogopa Mungu wananidhihaki kwa dharau,*Wananisagia meno yao.+ 17  Ee Yehova, utatazama tu mpaka lini?+ Niokoe dhidi ya mashambulizi yao,+Uhai wangu wenye thamani* kutoka kwa wanasimba.*+ 18  Kisha nitakushukuru katika kutaniko kubwa;+Nitakusifu katikati ya umati wa watu. 19  Usiruhusu wale ambao ni maadui wangu bila sababu wanicheke;Usiruhusu wale wanaonichukia bila sababu+ wakonyeze macho yao kwa hila.+ 20  Kwa maana hawasemi maneno ya amani,Lakini wanapanga njama kwa hila dhidi ya watu wenye amani nchini.+ 21  Wanafungua kinywa chao wazi ili wanishtaki,Wakisema: “Aha! Aha! Macho yetu yameliona.” 22  Ee Yehova, umeona jambo hilo. Usinyamaze.+ Ee Yehova, usikae mbali nami.+ 23  Amka, inuka unitetee,Mungu wangu, Yehova, nitetee katika kesi yangu. 24  Nihukumu kulingana na uadilifu wako,+ Ee Yehova Mungu wangu;Usiruhusu wanicheke. 25  Wasiseme kamwe moyoni mwao: “Aha! Tulipata tulichotaka!”* Wasiseme kamwe: “Tumemmeza.”+ 26  Acha wote waaibishwe na kufedheheshwa,Wale wanaonicheka kwa sababu ya msiba wangu. Acha wale wanaojikweza juu yangu wavishwe aibu na fedheha. 27  Lakini acha wale wanaofurahia uadilifu wangu wapaze sauti kwa shangwe;Na waseme daima: “Yehova na atukuzwe, anayefurahia amani ya mtumishi wake.”+ 28  Kisha ulimi wangu utasimulia* uadilifu wako+Na kukusifu mchana kutwa.+

Maelezo ya Chini

Kwa kawaida ilibebwa na wapiga mishale.
Au “shoka lenye makali pande zote mbili.”
Au “Iambie nafsi yangu.”
Au “wanaowinda nafsi yangu.”
Au “iliporudi kwenye kifua changu.”
Au labda, “Wasiomwogopa Mungu wanadhihaki ili wapate keki.”
Tnn., “Uhai pekee nilio nao,” yaani, nafsi yake.
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”
Au “Aha! Nafsi yetu.”
Au “utatafakari.”