Zaburi 36:1-12

  • Upendo mshikamanifu wa Mungu wenye thamani

    • Mwovu hamwogopi Mungu (1)

    • Mungu ni chanzo cha uhai (9)

    • “Kwa nuru yako tunaweza kuona nuru” (9)

Kwa kiongozi. Wa Daudi, mtumishi wa Yehova. 36  Dhambi huzungumza na mwovu ndani kabisa ya moyo wake;Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.+   Kwa maana hujisifusifu sana machoni pake mwenyeweHivi kwamba hawezi kutambua kosa lake na kulichukia.+   Maneno ya kinywa chake yanadhuru na ni ya udanganyifu;Haonyeshi ufahamu wowote wa kutenda mema.   Hupanga njama zinazodhuru hata kitandani mwake. Hufuatia njia isiyo njema;Hakatai lililo baya.   Ee Yehova, upendo wako mshikamanifu unafika mpaka mbinguni,+Uaminifu wako mpaka mawinguni.   Uadilifu wako ni kama milima mikubwa;*+Hukumu zako ni kama maji mengi yenye kina.+ Unawahifadhi* wanadamu na wanyama, Ee Yehova.+   Jinsi upendo wako mshikamanifu ulivyo na thamani sana, Ee Mungu!+ Katika kivuli cha mabawa yako,Wanadamu hukimbilia.+   Wanakunywa na kushiba vitu vinono vya* nyumba yako,+Nawe huwanywesha kwenye kijito cha vitu vyako vinavyofurahisha.+   Wewe ndiye chanzo cha uhai;+Kwa nuru yako tunaweza kuona nuru.+ 10  Endelea kuwatendea kwa upendo wako mshikamanifu wale wanaokujua,+Na kuwaonyesha uadilifu wako walio wanyoofu moyoni.+ 11  Usiruhusu mguu wa mwenye kiburi unikanyageWala mkono wa mwovu unifukuze. 12  Watenda maovu wameanguka huko;Wamepigwa na kuangushwa chini na hawawezi kusimama.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “kama milima ya Mungu.”
Au “Unawaokoa.”
Tnn., “mafuta ya.”