Zaburi 38:1-22

  • Sala ya mtu aliyetubu anayeteseka

    • “Nimesononeka na kushuka moyo kupita kiasi” (6)

    • Yehova huwasikia wale wanaomngojea (15)

    • “Nilihangaishwa na dhambi yangu” (18)

Muziki wa Daudi, wa kukumbusha. 38  Ee Yehova, usinikaripie kwa hasira yako,Wala usinirekebishe kwa ghadhabu yako.+   Kwa maana mishale yako imenichoma ndani kabisa,Na mkono wako unanikandamiza chini.+   Mwili wangu wote ni mgonjwa kwa sababu ya hasira yako kali. Hakuna amani katika mifupa yangu kwa sababu ya dhambi yangu.+   Kwa maana dhambi zangu zimetanda juu ya kichwa changu;+Kama mzigo mzito, ni nzito sana siwezi kuzibeba.   Vidonda vyangu vinanuka na vina usahaKwa sababu ya upumbavu wangu.   Nimesononeka na kushuka moyo kupita kiasi;Ninatembea huku na huku mchana kutwa kwa huzuni.   Ninaungua ndani ya mwili wangu;*Mwili wangu wote ni mgonjwa.+   Nimekufa ganzi na kupondeka kabisa;Moyo wangu wenye maumivu makali unanifanya nilie kwa sauti kubwa.*   Ee Yehova, unajua mambo yote ninayotamani,Na kilio changu cha maumivu hakijafichwa machoni pako. 10  Moyo wangu unadundadunda, nguvu zangu zimetoweka,Na nuru ya macho yangu imetoweka.+ 11  Rafiki zangu na wenzangu wananiepuka kwa sababu ya pigo langu,Na rafiki zangu wa karibu wanasimama mbali. 12  Wale wanaotafuta uhai wangu* wanatega mitego;Wale wanaojaribu kunidhuru wanazungumza kuhusu kuniangamiza;+Wananong’onezana uwongo mchana kutwa. 13  Lakini kama kiziwi, sikuwasikiliza;+Na kama bubu, sikufumbua kinywa changu.+ 14  Nimekuwa kama mtu asiyeweza kusikia,Ambaye kinywa chake hakina lolote la kujitetea. 15  Kwa maana nilikungojea wewe, Ee Yehova,+Nawe ukanijibu, Ee Yehova Mungu wangu.+ 16  Kwa maana nilisema: “Acha wasinichekeWala kujikweza juu yangu mguu wangu ukiteleza.” 17  Kwa maana nilikuwa karibu kuanguka,Na maumivu yangu yalikuwa pamoja nami daima.+ 18  Niliungama kosa langu;+Nilihangaishwa na dhambi yangu.+ 19  Lakini maadui wangu wana juhudi* na ni hodari,*Wale wanaonichukia bila sababu wameongezeka sana. 20  Walinilipa uovu kwa mema niliyotenda;Walinipinga kwa sababu ya kufuatia mambo mema. 21  Usiniache, Ee Yehova. Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami.+ 22  Njoo haraka unisaidie,Ee Yehova, wokovu wangu.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Viuno vyangu vimejaa moto.”
Au “ningurume.”
Au “nafsi yangu.”
Tnn., “wako hai.”
Au labda, “Lakini wale ambao ni maadui wangu bila sababu ni wengi.”