Zaburi 39:1-13

  • Ufupi wa maisha

    • Mwanadamu ni pumzi tu (5, 11)

    • “Usipuuze machozi yangu” (12)

Kwa kiongozi; wa Yeduthuni.*+ Muziki wa Daudi. 39  Nilisema: “Nitailinda hatua yanguIli niepuke kutenda dhambi kwa ulimi wangu.+ Nitakilinda kinywa changu kwa lijamu+Maadamu mtu yeyote mwovu yuko mbele yangu.”   Nilinyamaza na kukaa kimya;+Niliendelea kunyamaza hata kuhusu jambo jema,Lakini maumivu yangu yalikuwa makali.*   Moyo wangu uliteketea polepole* ndani yangu. Nilipokuwa nikiwaza sana,* moto huo uliendelea kuwaka. Kisha ulimi wangu ukasema:   “Ee Yehova, nisaidie kujua mwisho wangu,Na idadi ya siku zangu,+Ili nijue ufupi wa maisha yangu.*   Kwa kweli, umefanya siku zangu ziwe chache tu;*+Na urefu wa maisha yangu kuwa si kitu mbele zako.+ Kwa hakika kila mwanadamu, ingawa anaonekana yuko salama, si kitu ila pumzi tu.+ (Sela)   Kwa hakika kila mwanadamu hutembea huku na huku kama kivuli. Hukimbia huku na huku* bila sababu. Hurundika mali, bila kujua ni nani atakayeifurahia.+   Sasa basi, ninaweza kutumaini nini, Ee Yehova? Wewe ndiye tumaini langu pekee.   Niokoe kutoka katika makosa yangu yote.+ Usimruhusu mpumbavu anifanye kuwa kitu cha kudharauliwa.   Niliendelea kunyamaza;Sikuweza kufumbua kinywa changu,+Kwa maana wewe ndiye uliyefanya hayo.+ 10  Niondolee pigo lako. Nimedhoofika kabisa kwa sababu mkono wako unanipiga. 11  Unamrekebisha mwanadamu kwa kumwadhibu kwa sababu ya kosa lake;+Unaharibu kabisa vitu anavyothamini sana kama nondo* anavyoharibu. Kwa kweli kila mwanadamu ni pumzi tu.+ (Sela) 12  Sikia sala yangu, Ee Yehova,Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada.+ Usipuuze machozi yangu. Kwa maana kwako, mimi ni mkaaji mgeni tu,+Msafiri apitaye,* kama mababu zangu wote.+ 13  Usinitazame kwa ukali ili nichangamkeKabla sijafa* na kutoweka.”

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “yalichochewa.”
Tnn., “uliwaka moto.”
Au “nikipiga kite.”
Au “nijue jinsi ninavyopita upesi.”
Tnn., “ziwe vipimo vya mkono.”
Tnn., “Hupiga kelele.”
Aina fulani ya wadudu waharibifu.
Au “Mlowezi.”
Tnn., “sijapita.”