Zaburi 4:1-8

  • Sala ya kumtumaini Mungu

    • “Kasirika, lakini usitende dhambi” (4)

    • ‘Nitalala usingizi kwa amani’ (8)

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Muziki wa Daudi. 4  Ninapokuita, unijibu, Ee Mungu wangu mwadilifu.+ Nitengenezee njia ya kutoroka* taabu yangu. Nionyeshe kibali na usikie sala yangu.   Enyi wanadamu, mtaendelea mpaka lini kuibadili heshima yangu kuwa aibu? Mtaendelea mpaka lini kupenda mambo yasiyo na faida na kutafuta mambo ya uwongo? (Sela)   Jueni kwamba Yehova atamtendea mshikamanifu wake kwa njia ya pekee;*Yehova atasikia ninapomlilia.   Kasirika, lakini usitende dhambi.+ Zungumza moyoni mwako, kitandani mwako, na unyamaze kimya. (Sela)   Toa dhabihu za uadilifu,Na umtumaini Yehova.+   Kuna wengi wanaosema: “Ni nani atakayetuonyesha jambo lolote jema?” Acha nuru ya uso wako ituangazie, Ee Yehova.+   Umeujaza moyo wangu shangwe nyingi sanaKuliko wale walio na mavuno mengi sana ya nafaka na divai mpya.   Nitajilaza chini na kulala usingizi kwa amani,+Kwa maana wewe peke yako, Ee Yehova, hunifanya niishi kwa usalama.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “Nitengenezee nafasi pana katika.”
Au “atamfanya mshikamanifu wake aonekane kuwa tofauti; atamtenga kando mshikamanifu wake kwa ajili yake mwenyewe.”