Zaburi 40:1-17

  • Kumshukuru Mungu asiyeweza kulinganishwa na yeyote

    • Kazi za Mungu ni nyingi sana zisiweze kusimuliwa (5)

    • Dhabihu si jambo kuu kwa Mungu (6)

    • “Ninafurahia kufanya mapenzi yako” (8)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 40  Nilimtumaini Yehova kwa bidii,*Naye akanitegea sikio lake na kusikia* kilio changu cha kuomba msaada.+   Akanipandisha kutoka katika shimo linalonguruma,Kutoka katika matope yenye utelezi. Akaiweka miguu yangu juu ya jabali;Akanifanya nisimame mahali palipo imara.   Kisha akaweka wimbo mpya kinywani mwangu,+Asifiwe Mungu wetu. Wengi watatazama kwa hofuNa kumtumaini Yehova.   Mwenye furaha ni mtu anayemtumaini YehovaNa ambaye hawatumaini wakaidi au watu wadanganyifu.*   Jinsi ulivyotenda mambo mengi sana,Ee Yehova Mungu wangu,Kazi zako zinazostaajabisha na mawazo yako kutuelekea.+ Hakuna yeyote anayeweza kulinganishwa nawe;+Ikiwa ningejaribu kusimulia na kuongea kuzihusu,Zingekuwa nyingi sana kwangu kusimulia!+   Hukutamani* dhabihu na toleo,+Lakini ulifungua masikio yangu ili yasikie.+ Hukuomba dhabihu za kuteketezwa na dhabihu za dhambi.+   Kisha nikasema: “Tazama, nimekuja. Katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa kunihusu.+   Ee Mungu wangu, ninafurahia* kufanya mapenzi yako,+Na sheria yako imo ndani yangu kabisa.+   Ninatangaza habari njema ya uadilifu katika kutaniko kubwa.+ Tazama! Siizuii midomo yangu,+Ee Yehova, kama unavyojua vema. 10  Siufuniki uadilifu wako moyoni mwangu. Ninatangaza uaminifu wako na wokovu wako. Siufichi upendo wako mshikamanifu na ukweli wako katika kutaniko kubwa.”+ 11  Ee Yehova, usininyime rehema yako. Upendo wako mshikamanifu na ukweli wako na unilinde daima.+ 12  Misiba inayonizunguka ni mingi sana haihesabiki.+ Makosa yangu mengi yananilemea hivi kwamba siwezi kuona njia yangu;+Ni mengi sana kuliko nywele za kichwa changu,Nami nimevunjika moyo. 13  Tafadhali, Ee Yehova, uwe tayari kuniokoa.+ Ee Yehova, njoo haraka unisaidie.+ 14  Wote wanaotaka kuniua*Na waaibishwe na kufedheheshwa. Wale wanaofurahia msiba wanguNa wakimbie kwa aibu. 15  Wale wanaoniambia: “Aha! Aha!” Na washtuke kwa sababu ya aibu yao. 16  Lakini acha wale wanaokutafuta+Wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.+ Wale wanaopenda matendo yako ya wokovu na waseme daima: “Yehova na atukuzwe.”+ 17  Lakini sina uwezo, nami ni maskini;Yehova na anitunze. Wewe ni msaidizi wangu na mwokozi wangu;+Mungu wangu, usikawie.+

Maelezo ya Chini

Au “Nilimngojea Yehova kwa subira.”
Au “akainama chini ili kunisikiliza, akasikia.”
Au “waongo.”
Au “Hukupendezwa na.”
Au “ninatamani.”
Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”