Zaburi 41:1-13

  • Sala katika kitanda cha ugonjwa

    • Mungu huwategemeza wagonjwa (3)

    • Asalitiwa na rafiki wa karibu (9)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. 41  Mwenye furaha ni mtu yeyote anayemjali mtu wa hali ya chini;+Yehova atamwokoa siku ya msiba.   Yehova atamlinda na kumhifadhi hai. Atatangazwa kuwa mwenye furaha duniani;+Hutamtia kamwe mikononi mwa maadui wake ili wamtendee wapendavyo.*+   Yehova atamtegemeza kwenye kitanda chake cha ugonjwa;+Wakati huo wa ugonjwa utakibadili kabisa kitanda chake.   Kwa maana nilisema: “Ee Yehova, nionyeshe kibali.+ Niponye,*+ kwa maana nimekutendea dhambi.”+   Lakini maadui wangu wanasema mambo maovu kunihusu: “Atakufa lini jina lake litoweke?”   Mmoja wao akija kuniona, moyo wake husema uwongo. Hukusanya mambo yenye kudhuru ya kusema;Kisha hutoka nje na kuyaeneza kotekote.   Wote wanaonichukia wananong’onezana;Wanapanga njama ya uovu dhidi yangu:   “Amepatwa na jambo linaloogopesha;Sasa kwa kuwa yuko chini, hatainuka tena.”+   Hata mtu niliyekuwa na amani naye, ambaye nilimwamini,+Aliyekuwa akila mkate wangu, amekiinua kisigino chake dhidi yangu.*+ 10  Lakini wewe, Ee Yehova, nionyeshe kibali na kuniinua,Ili niwalipize. 11  Kwa njia hii nitajua kwamba unapendezwa nami: Adui yangu asipoweza kupaza sauti kwa ushindi dhidi yangu.+ 12  Lakini mimi, unanitegemeza kwa sababu ya utimilifu wangu;+Utaniweka mbele zako* milele.+ 13  Yehova, Mungu wa Israeli, na asifiweKwa umilele wote.*+ Amina na Amina.

Maelezo ya Chini

Au “Hutamtia kamwe katika tamaa ya maadui wake; au katika nafsi ya maadui wake.” Angalia Kamusi.
Au “Iponye nafsi yangu.”
Au “amenigeuka.”
Tnn., “mbele za uwepo wako.”
Au “Milele na milele.”