Zaburi 42:1-11

  • Kumsifu Mungu akiwa Mwokozi Mtukufu

    • Kuwa na kiu kwa ajili ya Mungu kama paa aliye na kiu ya maji (1, 2)

    • “Kwa nini nimesononeka?” (5, 11)

    • “Mngojee Mungu” (5, 11)

Kwa kiongozi. Maskili* ya wana wa Kora.+ 42  Kama paa anayetamani vijito vya maji,Ndivyo ninavyokutamani, Ee Mungu.   Nina kiu kwa ajili ya Mungu, kwa ajili ya Mungu aliye hai.+ Nije lini na kuonekana mbele za Mungu?+   Machozi yangu ni chakula changu usiku na mchana;Mchana kutwa watu wananidhihaki wakisema: “Mungu wako yuko wapi?”+   Ninayakumbuka mambo haya, nami naimwaga nafsi* yangu,Kwa maana wakati fulani nilitembea pamoja na umati;Nilikuwa nikitembea kimyakimya* mbele zao kwenda katika nyumba ya Mungu,Kwa sauti za shangwe na shukrani,Za umati unaofanya sherehe.+   Kwa nini nimesononeka?+ Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu? Mngojee Mungu,+Kwa maana bado nitamsifu kwa kuwa yeye ni Mwokozi wangu Mtukufu.+   Mungu wangu, nimesononeka.+ Ndiyo sababu ninakukumbuka,+Kutoka katika nchi ya Yordani na vilele vya Hermoni,Kutoka Mlima Mizari.*   Vilindi vya maji vinaita vilindi vya majiKwa sauti ya maporomoko yako ya maji. Mawimbi yako makubwa yamenilemea.+   Wakati wa mchana Yehova atanipa upendo wake mshikamanifu,Na usiku wimbo wake utakuwa pamoja nami—sala kwa Mungu wa uhai wangu.+   Nitamwambia Mungu, jabali langu: “Kwa nini umenisahau?+ Kwa nini nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?”+ 10  Maadui wangu wananidhihaki kwa chuki kali sana;** Mchana kutwa wananidhihaki wakisema: “Mungu wako yuko wapi?”+ 11  Kwa nini nimesononeka? Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu? Mngojee Mungu,+Kwa maana bado nitamsifu kwa kuwa yeye ni Mwokozi wangu Mtukufu na Mungu wangu.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “polepole.”
Au “ule mlima mdogo.”
Yaani, inayoweza kusababisha mauaji.
Au labda, “kana kwamba wanaiponda mifupa yangu.”