Zaburi 43:1-5

  • Mungu ambaye ni Mwamuzi huokoa

    • “Itume nuru yako na kweli yako” (3)

    • “Kwa nini nimesononeka?” (5)

    • “Mngojee Mungu” (5)

43  Nihukumu, Ee Mungu,+Itetee kesi yangu+ dhidi ya taifa lisilo na ushikamanifu. Niokoe kutoka kwa mtu mdanganyifu na asiye mwadilifu.   Kwa maana wewe ni Mungu wangu, ngome yangu.+ Kwa nini umenitupa? Kwa nini nitembee huku na huku nikiwa na huzuni kwa sababu ya kukandamizwa na adui yangu?+   Itume nuru yako na kweli yako.+ Navyo viniongoze;+Viniongoze kwenye mlima wako mtakatifu na kwenye hema lako tukufu la ibada.+   Kisha nitakuja kwenye madhabahu ya Mungu,+Kwa Mungu, shangwe yangu inayofurika. Nami nitakusifu kwa kinubi,+ Ee Mungu, Mungu wangu.   Kwa nini nimesononeka? Kwa nini msukosuko huu umo ndani yangu? Mngojee Mungu,+Kwa maana bado nitamsifu kwa kuwa yeye ni Mwokozi wangu Mtukufu na Mungu wangu.+

Maelezo ya Chini