Zaburi 44:1-26

  • Sala ya kuomba msaada

    • “Ni wewe uliyetuokoa” (7)

    • Kama “kondoo wa kuchinjwa” (22)

    • “Amka utusaidie!” (26)

Kwa kiongozi. Wa wana wa Kora.+ Maskili.* 44  Ee Mungu, tumesikia kwa masikio yetu wenyewe,Mababu zetu wametusimulia,+Mambo uliyotimiza katika siku zao,Siku za zamani za kale.   Kwa mkono wako uliyafukuza mataifa+Ukawafanya mababu zetu waishi huko.+ Uliyapondaponda mataifa na kuyafukuza.+   Hawakuimiliki nchi kwa upanga wao wenyewe,+Na mkono wao wenyewe haukuwaletea ushindi.+ Badala yake, waliimiliki kwa mkono wako wa kuume na uwezo wako+ na nuru ya uso wako,Kwa maana ulipendezwa nao.+   Wewe ni Mfalme wangu, Ee Mungu;+Amuru* ushindi kamili* kwa ajili ya Yakobo.   Kwa nguvu zako tutawafukuza maadui wetu;+Katika jina lako tutawakanyagia chini wale wanaoinuka dhidi yetu.+   Kwa maana siutumaini upinde wangu,Na upanga wangu hauwezi kuniokoa.+   Ni wewe uliyetuokoa kutoka kwa maadui wetu,+Wewe uliyewaaibisha wale wanaotuchukia.   Tutamsifu Mungu mchana kutwa,Nasi tutalishukuru jina lako milele. (Sela)   Lakini sasa umetutupa na kutuaibisha,Nawe huendi pamoja na majeshi yetu. 10  Unaendelea kutufanya tumkimbie adui yetu;+Wale wanaotuchukia wanachukua chochote wanachotaka. 11  Unatutia mikononi mwao ili tunyafuliwe kama kondoo;Umetutawanya miongoni mwa mataifa.+ 12  Unawauza watu wako kwa bei ya chini kabisa;+Hupati faida yoyote kwa kuwauza.* 13  Unatufanya kuwa shutuma kwa majirani wetu,Kitu cha kudhihakiwa na kufanyiwa mzaha na wale wote wanaotuzunguka. 14  Unatufanya kuwa kitu cha kudharauliwa* miongoni mwa mataifa,+Kitu cha kutikisiwa kichwa na mataifa. 15  Ninaaibika mchana kutwa,Nami nimelemewa na aibu yangu, 16  Kwa sababu ya sauti za wale wanaonidhihaki na kunitukana,Kwa sababu ya adui yetu anayelipiza kisasi. 17  Tumepatwa na mambo haya yote, lakini hatujakusahau,Wala hatujavunja agano lako.+ 18  Moyo wetu haujakengeuka;Hatua zetu hazitoki katika njia yako. 19  Lakini umetuponda mahali ambapo mbwamwitu wanakaa;Umetufunika kwa kivuli kizito. 20  Ikiwa tumelisahau jina la Mungu wetuAu ikiwa tutamnyooshea mungu wa kigeni mikono yetu tunaposali, 21  Je, Mungu hatagundua hilo? Anajua siri za moyo.+ 22  Kwa ajili yako tunauawa mchana kutwa;Tumehesabiwa kuwa kondoo wa kuchinjwa.+ 23  Amka. Kwa nini unaendelea kulala usingizi, Ee Yehova?+ Amka! Usiendelee kututupa milele.+ 24  Kwa nini unauficha uso wako? Kwa nini unasahau mateso yetu na kukandamizwa kwetu? 25  Kwa maana tumeshushwa chini mavumbini;Miili yetu imegandamizwa ardhini.+ 26  Amka utusaidie!+ Tuokoe* kwa sababu ya upendo wako mshikamanifu.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “Toa.”
Au “wokovu mkuu.”
Au “kutokana na bei yao.”
Tnn., “methali.”
Tnn., “Tukomboe.”