Zaburi 45:1-17

  • Ndoa ya mfalme mtiwa-mafuta

    • Maneno yenye fadhili (2)

    • “Mungu ni kiti chako cha ufalme milele” (6)

    • Mfalme anautamani urembo wa bibi harusi (11)

    • Wana watakuwa wakuu katika dunia yote (16)

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Wa wana wa Kora.+ Maskili.* Wimbo wa upendo. 45  Moyo wangu umesisimuliwa na jambo jema. Ninasema: “Wimbo wangu unamhusu* mfalme.”+ Ulimi wangu na uwe kalamu+ ya mnakili* stadi.+   Una sura nzuri kuliko wanadamu wote. Maneno yenye fadhili hutiririka kutoka katika midomo yako.+ Ndiyo sababu Mungu amekubariki milele.+   Jifunge upanga wako+ pajani, Ee mwenye nguvu,+Katika heshima na fahari yako.+   Na katika fahari yako endelea mpaka ushinde;*+Panda utetee kweli na unyenyekevu na uadilifu,+Na mkono wako wa kulia utatimiza* mambo yanayoogopesha.   Mishale yako ni mikali, inaangusha mataifa mbele yako;+Inachoma mioyo ya maadui wa mfalme.+   Mungu ni kiti chako cha ufalme milele na milele;+Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya unyoofu.*+   Ulipenda uadilifu+ na kuchukia uovu.+ Ndiyo sababu Mungu, Mungu wako, amekutia mafuta+ kwa mafuta ya kushangilia+ kuliko wenzako.   Mavazi yako yote yametiwa manukato ya manemane na udi na kida;Kutoka katika jumba tukufu la mfalme lililotengenezwa kwa pembe za tembo, vinanda vinakufanya ushangilie.   Mabinti wa wafalme ni miongoni mwa wanawake wako wanaoheshimiwa. Malkia amesimama mkono wako wa kulia, akiwa amepambwa kwa dhahabu ya Ofiri.+ 10  Sikiliza, Ee binti, sikiliza kwa makini na utege sikio lako;Wasahau watu wako na nyumba ya baba yako. 11  Naye mfalme atautamani urembo wako,Kwa maana yeye ni bwana wako,Kwa hiyo mwinamie. 12  Binti ya Tiro ataleta zawadi;Watu matajiri zaidi watatafuta kibali chako.* 13  Katika jumba la mfalme,* binti ya mfalme ana utukufu mwingi ajabu;Mavazi yake yamepambwa kwa* dhahabu. 14  Atapelekwa kwa mfalme akiwa na mavazi yaliyofumwa kwa ustadi mkubwa.* Mabikira wenzake wanaomfuata wanaletwa ndani mbele ya mfalme. 15  Wataletwa kwa furaha na shangwe;Wataingia katika jumba la mfalme. 16  Wana wako watachukua mahali pa mababu zako. Utawaweka kuwa wakuu katika dunia yote.+ 17  Nitalitangaza jina lako katika vizazi vyote vijavyo.+ Ndiyo sababu mataifa yatakusifu milele na milele.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Tnn., “Kazi zangu zinamhusu.”
Au “mwandishi.”
Tnn., “utakufundisha.”
Au “ufanikiwe.”
Au “haki.”
Au “watautuliza uso wako.”
Tnn., “Ndani.”
Tnn., “yametiwa mapambo ya.”
Au labda, “kwa majoho yaliyotariziwa.”