Zaburi 47:1-9

  • Mungu ni Mfalme wa dunia yote

    • ‘Yehova ni mwenye kuogopesha’ (2)

    • Mwimbieni Mungu sifa (6, 7)

Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+ 47  Enyi mataifa yote, pigeni makofi. Mpigieni Mungu kelele za ushindi kwa vigelegele vya shangwe.   Kwa maana Yehova, Aliye Juu Zaidi, ni mwenye kuogopesha;+Yeye ndiye Mfalme mkuu juu ya dunia yote.+   Huyatiisha mataifa chini yetu;Huyaweka mataifa chini ya miguu yetu.+   Hutuchagulia urithi wetu,+Fahari ya Yakobo, ambaye anampenda.+ (Sela)   Mungu amepanda juu kwa kelele za shangwe;Yehova, kwa sauti ya pembe.*   Mwimbieni Mungu sifa,* mwimbieni sifa. Mwimbieni sifa Mfalme wetu, mwimbieni sifa.   Kwa maana Mungu ni Mfalme wa dunia yote;+Mwimbieni sifa, na mwonyeshe ufahamu.   Mungu amekuwa Mfalme juu ya mataifa.+ Mungu huketi kwenye kiti chake kitakatifu cha ufalme.   Viongozi wa mataifa wamekusanyika pamojaPamoja na watu wa Mungu wa Abrahamu. Kwa maana watawala wa dunia ni wa* Mungu. Amekwezwa sana.+

Maelezo ya Chini

Au “pembe ya kondoo dume; tarumbeta.”
Au “Mpigieni Mungu muziki.”
Tnn., “ngao za dunia ni za.”