Zaburi 48:1-14

  • Sayuni, jiji la Mfalme Mtukufu

    • Shangwe ya dunia yote (2)

    • Likagueni jiji na minara yake (11-13)

Wimbo. Muziki wa wana wa Kora.+ 48  Yehova ni mkuu na anastahili kabisa kusifiwaKatika jiji la Mungu wetu, katika mlima wake mtakatifu.   Urefu wake unavutia, shangwe ya dunia yote,+Ni Mlima Sayuni ulio mbali sana kaskazini,Jiji la Mfalme Mkuu.+   Katika minara yake yenye ngome,Mungu ametangaza kwamba yeye ni kimbilio salama.*+   Kwa maana tazama! wafalme wamekusanyika;*Wamesonga mbele pamoja.   Walipoliona, walishangaa. Wakashikwa na wasiwasi na kukimbia kwa hofu.   Wakaanza kutetemeka wakiwa huko,Wakashikwa na uchungu kama wa mwanamke anayezaa.   Kwa upepo wa mashariki unavunjavunja meli za Tarshishi.   Mambo tuliyosikia, tumejionea wenyeweKatika jiji la Yehova wa majeshi, katika jiji la Mungu wetu. Mungu ataliimarisha kabisa milele.+ (Sela)   Tunautafakari upendo wako mshikamanifu, Ee Mungu,+Katika hekalu lako. 10  Kama jina lako, Ee Mungu, sifa yakoHufika mpaka kwenye miisho ya dunia.+ Mkono wako wa kuume umejaa uadilifu.+ 11  Mlima Sayuni+ na ushangilie,Miji ya Yuda na ishangilie,* kwa sababu ya hukumu zako.+ 12  Pigeni mwendo kuzunguka Sayuni; lizungukeni pande zote;Hesabuni minara yake.+ 13  Wekeni mioyo yenu juu ya maboma yake.*+ Kagueni minara yake yenye ngome,Ili msimulie vizazi vijavyo kulihusu. 14  Kwa maana Mungu huyu ni Mungu wetu+ milele na milele. Yeye mwenyewe atatuongoza kwa umilele wote.*+

Maelezo ya Chini

Au “kilele salama.”
Au “wamekutana kama walivyokubaliana.”
Tnn., “Mabinti wa Yuda na washangilie.”
Au “kuta zake zenye ngome.”
Au labda, “mpaka tufe.”