Zaburi 49:1-20

  • Upumbavu wa kuutumaini utajiri

    • Hakuna mwanadamu anayeweza kumkomboa mwingine (7, 8)

    • Mungu hukomboa kutoka Kaburini (15)

    • Utajiri hauwezi kuokoa kutoka katika kifo (16, 17)

Kwa kiongozi. Muziki wa wana wa Kora.+ 49  Sikieni hili, enyi mataifa yote. Sikilizeni, enyi wakaaji wote wa ulimwengu,*   Wakubwa kwa wadogo,*Matajiri na pia maskini.   Kinywa changu mwenyewe kitasema maneno ya hekima,Na kutafakari kwa moyo wangu+ kutaonyesha kwamba nina uelewaji.   Nitasikiliza methali;Nitategua kitendawili changu kwa kinubi.   Kwa nini niogope nyakati za taabu,+Ninapozungukwa na uovu wa* wale wanaojaribu kunipindua?   Wale wanaotumaini mali zao+Na kujigamba kuhusu utajiri wao mwingi,+   Hakuna yeyote kati yao anayeweza kamwe kumkomboa ndugu yakeWala kumpa Mungu fidia kwa ajili yake,+   (Bei ya fidia* kwa ajili ya uhai wao* ni yenye thamani sanaHivi kwamba hawawezi kamwe kulipa);   Ili kwamba aishi milele asilione shimo.*+ 10  Anaona kwamba hata watu wenye hekima hufa;Wapumbavu na wasiotumia akili huangamia pamoja,+Nao hulazimika kuwaachia wengine mali zao.+ 11  Ndani yao wanatamani nyumba zao zidumu milele,Mahema yao kizazi baada ya kizazi. Wameyaita mashamba yao kwa majina yao. 12  Lakini mwanadamu, ingawa anaheshimiwa, hataendelea kuishi;+Yeye si bora kuliko wanyama wanaoangamia.+ 13  Hiyo ndiyo njia ya wapumbavu+Na ya wale wanaowafuata, wanaofurahia maneno yao yasiyo na maana. (Sela) 14  Kama kondoo, wamepangiwa kwenda Kaburini.* Kifo kitawachunga;Wanyoofu watawatawala+ asubuhi. Kila sehemu ya mwili wao itatoweka kabisa;+Kaburi*+ litakuwa makao yao badala ya jumba la mfalme.+ 15  Lakini Mungu atanikomboa* kutoka katika nguvu za* Kaburi,*+Kwa maana atanishika. (Sela) 16  Usiogope mtu anapotajirika,Fahari ya nyumba yake ikiongezeka, 17  Kwa maana akifa hawezi kwenda na kitu chochote;+Fahari yake haitashuka shimoni pamoja naye.+ 18  Kwa maana wakati wa maisha yake anajipongeza mwenyewe.+ (Watu hukusifu unapopata ufanisi.)+ 19  Lakini mwishowe hujiunga na kizazi cha mababu zake. Hawataona nuru tena kamwe. 20  Mtu ambaye haelewi jambo hili, ingawa anaheshimiwa,+Yeye si bora kuliko wanyama wanaoangamia.

Maelezo ya Chini

Au “wa mfumo wa mambo.”
Tnn., “Wana wa wanadamu na pia wana wa mtu.”
Tnn., “kosa la.”
Au “ukombozi.”
Au “nafsi yao.”
Au “kaburi.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “mkono wa.”
Au “ataikomboa nafsi yangu.”