Zaburi 5:1-12

  • Yehova ni kimbilio la mwadilifu

    • Mungu anachukia uovu (4, 5)

    • ‘Niongoze katika uadilifu wako’ (8)

Kwa kiongozi wa Nehilothi.* Muziki wa Daudi. 5  Sikiliza maneno yangu, Ee Yehova;+Sikiliza kwa makini kilio changu cha uchungu.   Sikiliza kilio changu cha kuomba msaada,Ee Mfalme wangu na Mungu wangu, kwa sababu ninasali kwako.   Ee Yehova, utasikia sauti yangu asubuhi;+Asubuhi nitakueleza mahangaiko yangu+ na kusubiri kwa hamu.   Kwa maana wewe si Mungu anayefurahia uovu;+Hakuna mtu yeyote mwovu anayeweza kukaa nawe.+   Hakuna mtu yeyote mwenye kiburi anayeweza kusimama mbele zako.* Unawachukia wale wote wanaotenda maovu;+   Utawaangamiza wale wanaosema uwongo.+ Yehova anawachukia kabisa watu wakatili na wadanganyifu.*+   Lakini nitaingia katika nyumba yako+ kwa sababu ya upendo wako mwingi mshikamanifu;+Nitainama chini kuelekea hekalu lako takatifu* nikiwa na heshima na woga kukuelekea.+   Niongoze, Ee Yehova, katika uadilifu wako kwa sababu ya maadui wangu;Ifanye njia yako iwe wazi kwangu.+   Kwa maana hakuna lolote wanalosema linaloweza kutumainiwa;Ndani yao hamna lolote isipokuwa nia ya kudhuru. Koo lao ni kaburi lililo wazi;Wanasifusifu kwa ulimi wao.*+ 10  Lakini Mungu atawatangaza kuwa na hatia;Njama zao wenyewe zitasababisha waanguke.+ Na wafukuzwe kwa sababu ya dhambi zao nyingi,Kwa maana wamekuasi wewe. 11  Lakini wale wote wanaokukimbilia watashangilia;+Watapaza sauti kwa shangwe daima. Nawe utawakinga wasifikiwe,Na wale wanaolipenda jina lako watashangilia kwa sababu yako. 12  Kwa maana utambariki yeyote aliye mwadilifu, Ee Yehova;Utawazunguka kwa kibali kana kwamba kwa ngao kubwa.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Tnn., “katika uwepo wako.”
Au “anamchukia mtu anayemwaga damu na ambaye ni mdanganyifu.”
Au “mahali pako patakatifu.”
Au “Wanatumia ulimi laini.”