Zaburi 50:1-23

  • Mungu huhukumu kati ya mtu mshikamanifu na mwovu

    • Wanaofanya agano pamoja na Mungu kwa dhabihu (5)

    • “Mungu mwenyewe ni Mwamuzi” (6)

    • Wanyama wote ni wa Mungu (10, 11)

    • Mungu awafichua waovu (16-21)

Muziki wa Asafu.+ 50  Mungu wa miungu, Yehova,*+ amesema;Anaiita duniaKutoka mapambazuko ya jua mpaka machweo yake.*   Kutoka Sayuni, ukamilifu wa uzuri,+ Mungu huangaza.   Mungu wetu atakuja na hawezi kunyamaza.+ Mbele zake kuna moto unaoteketeza kabisa,+Na dhoruba kali inamzunguka pande zote.+   Anaziita mbingu zilizo juu na pia dunia,+Ili awahukumu watu wake:+   “Nikusanyieni washikamanifu wangu,Wale wanaofanya agano pamoja nami kwa dhabihu.”+   Mbingu zinatangaza uadilifu wake,Kwa maana Mungu mwenyewe ni Mwamuzi.+ (Sela)   “Sikilizeni, enyi watu wangu, nami nitaongea;Israeli, nitatoa ushahidi dhidi yako.+ Mimi ni Mungu, Mungu wako.+   Siwakaripii kwa sababu ya dhabihu zenu,Wala kwa sababu ya dhabihu zenu nzima za kuteketezwa ambazo daima ziko mbele zangu.+   Sihitaji kuchukua ng’ombe dume katika nyumba yako,Wala mbuzi* katika mazizi yako.+ 10  Kwa maana kila mnyama wa mwituni ni wangu,+Hata wanyama walio juu ya milima elfu moja. 11  Ninamjua kila ndege wa milimani;+Wanyama wasio na idadi wa mbugani ni wangu. 12  Ningekuwa na njaa, nisingekwambia,Kwa maana nchi inayozaa na kila kitu kilichomo ni changu.+ 13  Je, nitakula nyama ya ng’ombe dumeNa kunywa damu ya mbuzi?+ 14  Toa shukrani zikiwa dhabihu yako kwa Mungu,+Na utimize nadhiri zako kwa Aliye Juu Zaidi;+ 15  Nililie wakati wa taabu.+ Nitakuokoa, nawe utanitukuza.”+ 16  Lakini Mungu atamwambia mwovu: “Una haki gani ya kusimulia masharti yangu+Au kuongea kuhusu agano langu?+ 17  Kwa maana unachukia nidhamu,*Nawe unaendelea kuyageuzia mgongo maneno yangu.*+ 18  Unapomwona mwizi, unapendezwa naye,*+Nawe unashirikiana na wazinzi. 19  Unatumia kinywa chako kueneza mabaya,Na udanganyifu umeshikamana na ulimi wako.+ 20  Unaketi na kumsema vibaya ndugu yako mwenyewe;+Unafunua makosa ya* mwana wa mama yako mwenyewe. 21  Ulipofanya mambo hayo, niliendelea kunyamaza,Kwa hiyo ukafikiri kwamba nitakuwa kama wewe. Lakini sasa nitakukaripia,Nami nitatangaza kesi yangu dhidi yako.+ 22  Tafadhali, zingatieni jambo hili, ninyi mnaomsahau Mungu,+Nisije nikawararua vipandevipande asiwepo yeyote wa kuwaokoa. 23  Yule anayetoa shukrani kuwa dhabihu yake ananitukuza,+Na yule anayefuata njia iliyowekwa,Nitamfanya aone wokovu wa Mungu.”+

Maelezo ya Chini

Au “Yule Mungu, Yehova.”
Au “Kutoka mashariki mpaka magharibi.”
Tnn., “mbuzi dume.”
Tnn., “kuyatupa maneno yangu nyuma yako.”
Au “mafundisho.”
Au labda, “unaungana naye.”
Au “Unamharibia sifa.”