Zaburi 51:1-19

  • Sala ya mtu aliyetubu

    • Mwenye dhambi tangu alipochukuliwa mimba (5)

    • “Nisafishe kutoka katika dhambi yangu” (7)

    • “Umba moyo safi ndani yangu” (10)

    • Moyo uliopondeka humpendeza Mungu (17)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi, nabii Nathani alipokuja kwake baada ya Daudi kulala na Bath-sheba.+ 51  Ee Mungu, nionyeshe kibali kulingana na upendo wako mshikamanifu.+ Yafute kabisa makosa yangu kulingana na rehema zako nyingi.+   Nioshe kabisa kutoka katika kosa langu,+Na unisafishe kutoka katika dhambi yangu.+   Kwa maana ninajua vizuri makosa yangu,Na dhambi yangu iko mbele yangu* daima.+   Dhidi yako wewe—wewe zaidi ya wote*—nimetenda dhambi;+Nimetenda yaliyo mabaya machoni pako.+ Kwa hiyo, wewe ni mwadilifu unapoongea,Wewe ni mwenye haki katika hukumu yako.+   Tazama! Nilizaliwa nikiwa na hatia ya kosa,Na mama yangu alinichukua mimba katika dhambi.*+   Tazama! Unapendezwa na ukweli katika utu wa ndani;+Ufundishe utu wangu wa ndani kabisa* hekima ya kweli.   Nisafishe kutoka katika dhambi yangu kwa hisopo, ili niwe safi;+Nioshe, ili niwe mweupe kuliko theluji.+   Acha nisikie sauti za shangwe na furaha,Ili mifupa uliyoiponda ishangilie.+   Ugeuze uso wako* mbali na dhambi zangu,+Na uyafutilie mbali* makosa yangu yote.+ 10  Umba moyo safi ndani yangu, Ee Mungu,+Na uweke roho mpya ndani yangu,+ iliyo imara. 11  Usinitupe kutoka mbele zako;*Wala usiniondolee roho yako takatifu. 12  Nirudishie shangwe ya wokovu wako;+Chochea ndani yangu utayari wa kukutii.* 13  Nitawafundisha wakosaji njia zako,+Ili watenda dhambi wakurudie. 14  Niokoe kutoka katika hatia ya damu,+ Ee Mungu, Mungu wa wokovu wangu,+Ili ulimi wangu utangaze uadilifu wako kwa shangwe.+ 15  Ee Yehova, ifungue midomo yangu,Ili kinywa changu kitangaze sifa yako.+ 16  Kwa maana hutaki dhabihu—la sivyo ningeitoa;+Hupendezwi na dhabihu nzima ya kuteketezwa.+ 17  Dhabihu zinazompendeza Mungu ni roho iliyovunjika;Moyo uliovunjika na kupondeka, Ee Mungu, hutaukataa.*+ 18  Kwa nia yako njema litendee jiji la Sayuni jambo jema;Zijenge kuta za Yerusalemu. 19  Ndipo utakapopendezwa na dhabihu za uadilifu,Dhabihu za kuteketezwa na matoleo mazima;Kisha ng’ombe dume watatolewa kwenye madhabahu yako.+

Maelezo ya Chini

Au “akilini mwangu.”
Tnn., “wewe peke yako.”
Au “Na nilikuwa na dhambi tangu mama yangu aliponichukua mimba.”
Au “utu wangu wa sirini.”
Au “Ufiche uso wako.”
Au “uyafute kabisa.”
Tnn., “mbele za uwepo wako.”
Tnn., “Nitegemeze kwa kunipa roho ya utayari.”
Au “hutaudharau.”