Zaburi 52:1-9

  • Kuutumaini upendo mshikamanifu wa Mungu

    • Wanaojigamba kwa sababu ya uovu waonywa (1-5)

    • Wasiomwogopa Mungu wanautumaini utajiri (7)

Kwa kiongozi. Maskili.* Wa Daudi, Doegi Mwedomu alipokuja na kumwambia Sauli kwamba Daudi alikuwa ameenda kwenye nyumba ya Ahimeleki.+ 52  Kwa nini unajigamba kuhusu matendo yako maovu, ewe mwenye nguvu?+ Upendo mshikamanifu wa Mungu unadumu mchana kutwa.+   Ulimi wako, wenye makali kama wembe,+Hupanga madhara na kutunga mambo ya udanganyifu.+   Unapenda uovu kuliko mema,Kusema uwongo kuliko kusema ukweli. (Sela)   Unapenda kila neno linalodhuru,Ewe ulimi mdanganyifu!   Ndiyo sababu Mungu atakubomoa milele na milele;+Atakunyakua na kukurarua kutoka katika hema lako;+Atakung’oa kutoka katika nchi ya walio hai.+ (Sela)   Waadilifu wataona jambo hilo na kujawa na woga,+Nao watamcheka.+   “Huyu ndiye mwanamume ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake,*+Lakini aliutumaini utajiri wake mwingi+Na kutegemea* njama zake mwenyewe za uovu.”*   Lakini mimi nitakuwa kama mzeituni wenye majani mengi katika nyumba ya Mungu;Ninautumaini upendo mshikamanifu wa Mungu,+ milele na milele.   Nitakusifu milele kwa sababu umechukua hatua;+Mbele ya washikamanifu wako,Nitalitumaini jina lako,+ kwa maana ni jema.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “ngome yake.”
Au “kujificha katika.”
Tnn., “taabu anazosababisha.”