Zaburi 53:1-6

  • Ufafanuzi kumhusu mpumbavu

    • “Hakuna Yehova” (1)

    • “Hakuna yeyote anayetenda mema” (3)

Kwa kiongozi; katika mtindo wa Mahalathi.* Maskili.* Wa Daudi. 53  Mpumbavu* husema moyoni mwake: “Hakuna Yehova.”+ Matendo yao maovu yamepotoka na yanachukiza;Hakuna yeyote anayetenda mema.+   Lakini Mungu anawatazama wanadamu kutoka mbinguni+Ili aone ikiwa kuna yeyote aliye na ufahamu, ikiwa kuna yeyote anayemtafuta Yehova.+   Wote wamekengeuka;Wote wamepotoka. Hakuna yeyote anayetenda mema,Hakuna hata mmoja.+   Je, hakuna mtenda maovu yeyote anayeelewa? Wanawala watu wangu kwa pupa kana kwamba wanakula mkate. Hawamwiti Yehova.+   Lakini watajawa na hofu kubwa,Hofu ambayo hawajawahi kamwe kuwa nayo,*Kwa maana Mungu ataitawanya mifupa ya wale wanaowashambulia ninyi.* Mtawaaibisha, kwa maana Yehova amewakataa wao.   Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+ Yehova anapowakusanya tena watu wake waliotekwa,Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Angalia Kamusi.
Au “Asiye na akili.”
Au labda, “Hofu mahali pasipo na chochote cha kuhofu.”
Tnn., “wanaopiga kambi dhidi yenu.”