Zaburi 53:1-6
Kwa kiongozi; katika mtindo wa Mahalathi.* Maskili.* Wa Daudi.
53 Mpumbavu* husema moyoni mwake:
“Hakuna Yehova.”+
Matendo yao maovu yamepotoka na yanachukiza;Hakuna yeyote anayetenda mema.+
2 Lakini Mungu anawatazama wanadamu kutoka mbinguni+Ili aone ikiwa kuna yeyote aliye na ufahamu, ikiwa kuna yeyote anayemtafuta Yehova.+
3 Wote wamekengeuka;Wote wamepotoka.
Hakuna yeyote anayetenda mema,Hakuna hata mmoja.+
4 Je, hakuna mtenda maovu yeyote anayeelewa?
Wanawala watu wangu kwa pupa kana kwamba wanakula mkate.
Hawamwiti Yehova.+
5 Lakini watajawa na hofu kubwa,Hofu ambayo hawajawahi kamwe kuwa nayo,*Kwa maana Mungu ataitawanya mifupa ya wale wanaowashambulia ninyi.*
Mtawaaibisha, kwa maana Yehova amewakataa wao.
6 Laiti wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+
Yehova anapowakusanya tena watu wake waliotekwa,Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi.