Zaburi 54:1-7

  • Sala ya kuomba msaada unapokuwa kati ya maadui

    • “Mungu ni msaidizi wangu” (4)

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Maskili.* Wa Daudi, Wazifu walipokuja na kumwambia Sauli: “Daudi anajificha miongoni mwetu.”+ 54  Ee Mungu, niokoe kwa jina lako,+Na unitetee*+ kwa nguvu zako.   Ee Mungu, isikie sala yangu;+Sikiliza maneno ya kinywa changu.   Kwa maana wageni wanainuka dhidi yangu,Na wanaume wakatili wanatafuta uhai wangu.*+ Hawamheshimu Mungu.*+ (Sela)   Tazama! Mungu ni msaidizi wangu;+Yehova yuko pamoja na wale wanaonitegemeza.   Utawalipa maadui wangu+ uovu wao wenyewe;Katika uaminifu wako, waangamize.*+   Nitakutolea dhabihu+ kwa hiari. Nitalisifu jina lako, Ee Yehova, kwa maana ni jema.+   Kwa maana wewe huniokoa kutoka katika kila taabu,+Nami nitawatazama maadui wangu wakishindwa.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “uamue kesi yangu.”
Au “nafsi yangu.”
Au “Hawamweki Mungu mbele yao.”
Tnn., “wanyamazishe.”