Zaburi 56:1-13

  • Sala ya mtu anayeteswa

    • “Katika Mungu ninaweka tumaini langu” (4)

    • “Machozi yangu katika kiriba chako cha ngozi” (8)

    • “Mwanadamu ambaye ni duni tu atanifanya nini?” (4, 11)

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Njiwa Mnyamavu Aliye Mbali.” Wa Daudi. Miktamu.* Wafilisti walipomkamata kule Gathi.+ 56  Nionyeshe kibali, Ee Mungu, kwa sababu mwanadamu anayeweza kufa ananishambulia.* Mchana kutwa wanaendelea kunipiga vita na kunikandamiza.   Maadui wangu wanajaribu mchana kutwa kuning’ata;Wengi wanapigana nami kwa kiburi.   Ninapoogopa,+ ninakutumaini wewe.+   Katika Mungu—ninayelisifu neno lake—Katika Mungu ninaweka tumaini langu; siogopi. Mwanadamu ambaye ni duni tu atanifanya* nini?+   Mchana kutwa wanavuruga mambo yangu;Jambo pekee wanalowazia ni kunidhuru.+   Wanajificha ili wanishambulie,Wanachunguza kila hatua yangu,+Wakikusudia kuuondoa uhai wangu.+   Wakatae kwa sababu ya uovu wao. Yaangushe mataifa kwa hasira yako, Ee Mungu.+   Unafuatia kutangatanga kwangu.+ Yakusanye machozi yangu katika kiriba chako cha ngozi.+ Je, hayajaandikwa katika kitabu chako?+   Maadui wangu watakimbia siku nitakayoomba msaada.+ Nina hakika kuhusu jambo hili: Mungu yuko upande wangu.+ 10  Katika Mungu—ninayelisifu neno lake—Katika Yehova—ninayelisifu neno lake— 11  Katika Mungu ninaweka tumaini langu; siogopi.+ Mwanadamu ambaye ni duni tu atanifanya nini?+ 12  Nimefungwa na nadhiri nilizokuwekea, Ee Mungu;+Nitakutolea matoleo ya shukrani.+ 13  Kwa maana umeniokoa kutoka katika kifo+Na kuizuia miguu yangu isijikwae,+Ili nitembee mbele za Mungu katika nuru ya walio hai.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “anataka kuning’ata.”
Tnn., “Mwili wa nyama utanifanya.”