Zaburi 57:1-11

  • Sala ya kuomba kibali

    • Kimbilio chini ya mabawa ya Mungu (1)

    • Maadui waanguka katika mtego wao wenyewe (6)

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.* Alipomkimbia Sauli na kuingia pangoni.+ 57  Nionyeshe kibali, Ee Mungu, nionyeshe kibali,Kwa maana ninakukimbilia,+Ninakimbilia kivuli cha mabawa yako mpaka matatizo haya yapite.+   Ninamlilia Mungu Aliye Juu Zaidi,Mungu wa kweli, anayeyakomesha kwa ajili yangu.   Atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa.+ Atamtamausha yule anayejaribu kuning’ata. (Sela) Mungu atatuma upendo wake mshikamanifu na uaminifu wake.+   Nimezungukwa na simba;+Nimelazimika kulala miongoni mwa watu wanaotaka kuninyafua,Ambao meno yao ni mikuki na mishaleNa ambao ulimi wao ni upanga mkali.+   Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+   Wameutayarisha wavu ili kuinasa miguu yangu;+Taabu zimenifanya niiname chini.+ Wamechimba shimo mbele yangu,Lakini wao wenyewe wameanguka ndani yake.+ (Sela)   Moyo wangu uko imara, Ee Mungu,+Moyo wangu uko imara. Nitaimba na kupiga muziki.   Amka, utukufu wangu. Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi. Nitayaamsha mapambazuko.+   Nitakusifu miongoni mwa mataifa, Ee Yehova;+Nitakuimbia sifa* miongoni mwa mataifa.+ 10  Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkubwa, uko juu kama mbingu,+Na uaminifu wako, unafika mpaka angani. 11  Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “Nitakupigia muziki.”