Zaburi 58:1-11

  • Kuna Mungu anayeihukumu dunia

    • Sala ya kuomba waovu waadhibiwe (6-8)

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.* 58  Je, mnaweza kuzungumza kuhusu uadilifu wakati mmenyamaza?+ Je, mnaweza kuhukumu kwa unyoofu, enyi wanadamu?+   Badala yake, mnatunga uovu moyoni mwenu,+Na mikono yenu inatawanya ukatili nchini.+   Waovu wanakengeuka* tangu kuzaliwa;Ni wakaidi, waongo tangu wanapozaliwa.   Sumu yao ni kama sumu ya nyoka;+Wao ni viziwi kama swila anayeziba sikio lake.   Hataisikiliza sauti ya wanaomchezesha,Hata wafanye uchawi kwa ustadi kadiri gani.   Ee Mungu, yavunje meno yao vinywani mwao! Yavunje mataya ya hawa simba,* Ee Yehova!   Na watoweke kama maji yanayotiririka na kwenda zake. Mungu na aukunje upinde wake na kuwaangusha kwa mishale yake.   Na wawe kama konokono anayeyeyuka anapotembea;Kama mtoto anayefia tumboni mwa mwanamke, mtoto asiyeona jua kamwe.   Kabla vyungu vyenu vya kupikia havijapata moto wa kuni za mkwamba,Atazifagilia mbali kuni zenye unyevu na zinazowaka moto, kama kwa kimbunga.+ 10  Mwadilifu atashangilia kwa sababu ameona kisasi;+Miguu yake italowa damu ya waovu.+ 11  Kisha watu watasema: “Kwa hakika kuna thawabu kwa ajili ya mwadilifu.+ Kwa hakika kuna Mungu anayehukumu duniani.”+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “wamepotoka.”
Au “wanasimba wenye manyoya marefu shingoni.”