Zaburi 59:1-17

  • Mungu ni ngao na kimbilio

    • “Usiwaonyeshe rehema wasaliti” (5)

    • “Nitaimba kuhusu nguvu zako” (16)

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Usiharibu.” Wa Daudi. Miktamu.* Sauli alipowatuma watu waichunguze nyumba ya Daudi* ili wamuue.+ 59  Niokoe kutoka kwa maadui wangu, Ee Mungu wangu;+Nilinde kutoka kwa wale wanaoinuka dhidi yangu.+   Niokoe kutoka kwa wale wanaotenda uovu,Na uniokoe kutoka kwa watu wakatili.*   Tazama! Wananivizia;+Wanaume wenye nguvu wananishambuliaLakini si kwa sababu nimeasi au kutenda dhambi,+ Ee Yehova.   Ingawa sikutenda kosa lolote, wanakimbia na kujitayarisha kunishambulia. Inuka ninapokuita, uone.   Kwa maana wewe, Ee Yehova Mungu wa majeshi, ni Mungu wa Israeli.+ Amka uyakazie uangalifu mataifa yote. Usiwaonyeshe rehema wasaliti wowote wenye nia ya kudhuru.+ (Sela)   Wanarudi kila jioni;+Wanabweka* kama mbwa+ na kuzungukazunguka jijini.+   Tazama kinachomwagika* kutoka katika kinywa chao;Midomo yao ni kama panga,+Kwa maana wanauliza: “Ni nani anayesikiliza?”+   Lakini wewe, Ee Yehova, utawacheka;+Utayadhihaki mataifa yote.+   Ee Nguvu zangu, nitaendelea kukutarajia;+Kwa maana Mungu ni kimbilio langu salama.*+ 10  Mungu anayenitendea kwa upendo mshikamanifu atanisaidia;+Mungu ataniwezesha niwatazame maadui wangu wakishindwa.+ 11  Usiwaue, ili watu wangu wasisahau. Kwa nguvu zako wafanye watangetange;Waangushe, Ee Yehova, ngao yetu.+ 12  Kwa sababu ya dhambi ya kinywa chao, neno la midomo yao,Kiburi chao na kiwanase,+Kwa sababu ya matusi na udanganyifu wanaosema. 13  Waangamize kwa hasira yako kali;+Waangamize kabisa, ili wasiwepo tena;Wafanye wajue kwamba Mungu anatawala katika Yakobo na mpaka kwenye miisho ya dunia.+ (Sela) 14  Acha warudi jioni;Acha wabweke* kama mbwa na kuzungukazunguka jijini.+ 15  Acha watangetange wakitafuta chakula;+Usiwaruhusu washibe au kupata makao. 16  Lakini mimi, nitaimba kuhusu nguvu zako;+Asubuhi nitatangaza kwa shangwe kuhusu upendo wako mshikamanifu. Kwa maana wewe ni kimbilio langu salama+Na mahali pangu pa kukimbilia wakati wa taabu.+ 17  Ee Nguvu zangu, nitakuimbia sifa,*+Kwa maana wewe Mungu ni kimbilio langu salama, Mungu unayenitendea kwa upendo mshikamanifu.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Tnn., “waichunguze ile nyumba.”
Au “wenye kiu ya damu.”
Au “Wananguruma.”
Au “kinachobubujika.”
Au “kilele changu salama.”
Au “wangurume.”
Au “nitakupigia muziki.”