Zaburi 6:1-10

  • Ombi la kupata kibali

    • Waliokufa hawamsifu Mungu (5)

    • Mungu husikia sala za kuomba kibali (9)

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda vilivyopatanishwa na sauti ya Sheminithi.* Muziki wa Daudi. 6  Ee Yehova, usinikaripie katika hasira yako,Na usinirekebishe katika ghadhabu yako.+   Nionyeshe kibali,* Ee Yehova, kwa maana ninadhoofika. Niponye, Ee Yehova,+ kwa maana mifupa yangu inatetemeka.   Naam, ninasumbuka* sana,+Nami nakuuliza, Ee Yehova—nitasumbuka mpaka lini?+   Rudi, Ee Yehova, uniokoe;*+Niokoe kwa ajili ya upendo wako mshikamanifu.+   Kwa maana waliokufa hawakutaji;*Katika kaburi,* ni nani atakayekusifu?+   Nimechoka kwa sababu ya kulia kwa uchungu;+Usiku kucha ninakilowesha kitanda changu kwa machozi;*Kochi langu nalifanya lifurike kwa machozi.+   Jicho langu limedhoofika kwa sababu ya huzuni yangu;+Limeingia giza* kwa sababu ya wote wanaoninyanyasa.   Niondokeeni, ninyi nyote mnaotenda maovu,Kwa maana Yehova atasikia sauti ya kilio changu.+   Yehova atasikia ombi langu la kutaka kibali;+Yehova ataikubali sala yangu. 10  Maadui wangu wote wataaibishwa na kutamaushwa;Watarudi nyuma ghafla kwa aibu.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “rehema.”
Au “nafsi yangu inasumbuka.”
Au “uiokoe nafsi yangu.”
Au “hawakukumbuki.”
Au “Sheoli.” Angalia Kamusi.
Tnn., “ninakifanya kitanda changu kiogelee.”
Au “Limezeeka.”