Zaburi 60:1-12

  • Mungu huwatiisha maadui

    • Wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote (11)

    • “Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu” (12)

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Yungiyungi la Kikumbusho.” Miktamu.* Wa Daudi. Wa kufundisha. Alipopigana na Aram-naharaimu na Aram-Soba, kisha Yoabu akarudi na kuwaua Waedomu 12,000 katika Bonde la Chumvi.+ 60  Ee Mungu, ulitukataa; ulipenya katika vikosi vyetu vya ulinzi.+ Ulitukasirikia; lakini sasa tupokee tena!   Uliifanya dunia itetemeke; uliipasua ikafunguka. Ziba nyufa zake, kwa maana inaporomoka.   Uliwafanya watu wako wateseke. Ulitufanya tunywe divai inayosababisha tuyumbeyumbe.+   Wape* ishara wale wanaokuogopaWakimbie na kuukwepa upinde. (Sela)   Ili wapendwa wako waokolewe,Tuokoe kwa mkono wako wa kuume na utujibu.+   Mungu ameongea katika utakatifu wake:* “Nitashangilia, nitawagawia Shekemu kuwa urithi,+Nami nitawapimia Bonde la* Sukothi.+   Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu,+Na Efraimu ni kofia ya kukinga* kichwa changu;Yuda ni fimbo yangu ya kiongozi.+   Moabu ni beseni langu la kuogea.+ Nitatupa kiatu changu juu ya Edomu.+ Nitapaza sauti kwa ushindi juu ya Ufilisti.”+   Ni nani atakayenipeleka kwenye jiji lililozingirwa?* Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?+ 10  Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetukataa,Mungu wetu, ambaye haendi tena na majeshi yetu?+ 11  Tusaidie katika taabu yetu,Kwa maana wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote.+ 12  Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu,+Naye atawakanyagia chini maadui wetu.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au labda, “Umewapa.”
Au labda, “mahali pake patakatifu.”
Au “Nchi Tambarare ya Chini ya.”
Tnn., “ngome ya.”
Au labda, “lenye ngome.”