Zaburi 61:1-8
-
Mungu ni mnara wenye nguvu dhidi ya maadui
-
“Nitakuwa mgeni katika hema lako” (4)
-
Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Wa Daudi.
61 Ee Mungu, sikia kilio changu cha kuomba msaada.
Sikiliza sala yangu.+
2 Nitakulilia kwa sauti kutoka katika miisho ya duniaNinapovunjika moyo.*+
Niongoze kwenye mwamba ulio juu kuliko mimi.+
3 Kwa maana wewe ni kimbilio langu,Mnara ulio imara unaonilinda dhidi ya adui.+
4 Nitakuwa mgeni katika hema lako milele;+Nitakimbilia katika kivuli cha mabawa yako.+ (Sela)
5 Kwa maana wewe, Ee Mungu, umesikia nadhiri zangu.
Umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.+
6 Utamwongezea mfalme siku za maisha yake,+Na miaka yake itatoka kizazi hadi kizazi.
7 Ataketi kwenye kiti cha ufalme* milele mbele za Mungu;+Mpe upendo wako mshikamanifu na uaminifu, ili vimlinde.+
8 Kisha nitaliimbia sifa* jina lako milele+Ninapotimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.+