Zaburi 61:1-8

  • Mungu ni mnara wenye nguvu dhidi ya maadui

    • “Nitakuwa mgeni katika hema lako” (4)

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Wa Daudi. 61  Ee Mungu, sikia kilio changu cha kuomba msaada. Sikiliza sala yangu.+   Nitakulilia kwa sauti kutoka katika miisho ya duniaNinapovunjika moyo.*+ Niongoze kwenye mwamba ulio juu kuliko mimi.+   Kwa maana wewe ni kimbilio langu,Mnara ulio imara unaonilinda dhidi ya adui.+   Nitakuwa mgeni katika hema lako milele;+Nitakimbilia katika kivuli cha mabawa yako.+ (Sela)   Kwa maana wewe, Ee Mungu, umesikia nadhiri zangu. Umenipa urithi wa wale wanaoliogopa jina lako.+   Utamwongezea mfalme siku za maisha yake,+Na miaka yake itatoka kizazi hadi kizazi.   Ataketi kwenye kiti cha ufalme* milele mbele za Mungu;+Mpe upendo wako mshikamanifu na uaminifu, ili vimlinde.+   Kisha nitaliimbia sifa* jina lako milele+Ninapotimiza nadhiri zangu siku baada ya siku.+

Maelezo ya Chini

Au “Moyo wangu unapodhoofika.”
Au “Atakaa.”
Au “nitalipigia muziki.”