Zaburi 62:1-12

  • Wokovu wa kweli hutoka kwa Mungu

    • “Ninamngojea Mungu kimyakimya” (1, 5)

    • ‘Mwageni mioyo yenu mbele za Mungu’ (8)

    • Wanadamu ni pumzi tu (9)

    • Usitumaini mali (10)

Kwa kiongozi; wa Yeduthuni.* Muziki wa Daudi. 62  Kwa kweli, ninamngojea Mungu kimyakimya. Wokovu wangu unatoka kwake.+   Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;*+Kamwe, sitatikiswa sana.+   Mtaendelea mpaka lini kumshambulia mtu ili kumuua?+ Ninyi nyote ni hatari kama ukuta ulioinama, ukuta wa mawe unaokaribia kuanguka.*   Kwa maana wanashauriana ili kumwangusha kutoka katika cheo chake cha juu;*Wanafurahia kusema uwongo. Kwa kinywa chao wanabariki, lakini ndani yao wanalaani.+ (Sela)   Kwa kweli, ninamngojea* Mungu kimyakimya+Kwa sababu tumaini langu linatoka kwake.+   Kwa kweli, yeye ni mwamba wangu na wokovu wangu, kimbilio langu salama;Sitatikiswa kamwe.+   Wokovu wangu na utukufu wangu unamtegemea Mungu. Mwamba wangu imara, kimbilio langu, ni Mungu.+   Mtumainini nyakati zote, enyi watu. Mwageni mioyo yenu mbele zake.+ Mungu ni kimbilio letu.+ (Sela)   Wanadamu ni pumzi tu,Wana wa binadamu ni njozi ya uwongo.+ Wanapowekwa pamoja kwenye mizani, ni wepesi kuliko pumzi.+ 10  Msitegemee upunjajiWala kuwa na matumaini ya uwongo katika unyang’anyi. Mali zako zikiongezeka, usizikazie moyoni mwako.+ 11  Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimelisikia jambo hili: Kwamba nguvu ni za Mungu.+ 12  Pia upendo mshikamanifu ni wako, Ee Yehova,+Kwa maana unamlipa kila mtu kulingana na matendo yake.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “kilele changu salama.”
Au labda, “Ninyi nyote, kana kwamba alikuwa ukuta ulioinama, ukuta wa mawe unaokaribia kuanguka.”
Au “heshima yake.”
Au “Kwa kweli, Ee nafsi yangu, mngojee.”