Zaburi 63:1-11

  • Kumtamani Mungu

    • “Upendo wako mshikamanifu ni bora kuliko uhai” (3)

    • “Nimeridhika na fungu bora” (5)

    • Kutafakari kumhusu Mungu wakati wa usiku (6)

    • ‘Ninashikamana na Mungu’ (8)

Muziki wa Daudi, alipokuwa katika nyika ya Yuda.+ 63  Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, ninaendelea kukutafuta.+ Nina kiu kwa ajili yako.+ Ninazimia* kwa sababu ninakutamaniKatika nchi kame iliyokauka, ambayo haina maji.+   Kwa hiyo nimekutazama mahali patakatifu;Nimeziona nguvu zako na utukufu wako.+   Kwa sababu upendo wako mshikamanifu ni bora kuliko uhai,+Midomo yangu mwenyewe itakutukuza.+   Basi nitakusifu maisha yangu yote;Katika jina lako nitaiinua mikono yangu.   Nimeridhika na fungu bora ambalo ni zuri kabisa,*Kwa hiyo kinywa changu kitakusifu kwa midomo yenye shangwe.+   Ninakukumbuka wewe nikiwa kitandani mwangu;Ninatafakari kukuhusu katika makesha ya usiku.+   Kwa maana wewe ni msaidizi wangu,+Nami ninapaza sauti kwa shangwe katika kivuli cha mabawa yako.+   Ninashikamana nawe;Mkono wako wa kuume hunishika kwa nguvu.+   Lakini wale wanaotaka kuniua*Watashuka katika sehemu zenye kina zaidi za dunia. 10  Watatiwa katika nguvu za upanga;Watakuwa chakula cha mbwamwitu.* 11  Lakini mfalme atashangilia kwa sababu ya Mungu. Kila mtu anayeapa katika jina la Mungu atashangilia,*Kwa maana kinywa cha wale wanaosema uwongo kitanyamazishwa.

Maelezo ya Chini

Tnn., “Mwili wangu unazimia.”
Tnn., “Nimeridhika kana kwamba nina mafuta na nimejaa mafuta.”
Au “kuiangamiza nafsi yangu.”
Au “mbweha.”
Au “atajigamba.”