Zaburi 65:1-13

  • Mungu anaitunza dunia

    • “Msikiaji wa sala” (2)

    • “Mwenye furaha ni yule unayemchagua” (4)

    • Wema mwingi wa Mungu (11)

Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi. Wimbo. 65  Ee Mungu, sifa inakungojea Sayuni;+Tutatimiza nadhiri zetu kwako.+   Ee Msikiaji wa sala, watu wa kila aina* watakujia.+   Dhambi zangu zimenilemea,+Lakini unafunika makosa yetu.+   Mwenye furaha ni yule unayemchagua na kumleta karibuIli akae katika nyua zako.+ Tutaridhika na wema wa nyumba yako,+Hekalu lako takatifu.*+   Utatujibu kwa matendo ya uadilifu yanayoogopesha,+Ee Mungu wa wokovu wetu;Wewe ndiye Tegemeo la miisho yote ya dunia+Na wa wale walio mbali ng’ambo ya bahari.   Uliimarisha kabisa milima kwa nguvu zako;Umevaa uwezo.+   Unazituliza bahari zilizochafuka,+Kishindo cha mawimbi yake na msukosuko wa mataifa.+   Wale wanaokaa sehemu za mbali wataogopeshwa na ishara zako;+Utawafanya wale wanaoishi upande wa mashariki mpaka upande wa magharibi wapaze sauti kwa shangwe.   Unaitunza dunia,Unaifanya izae kwa wingi* na kuitajirisha sana.+ Kijito kinachotoka kwa Mungu kimejaa maji;Unawapa nafaka,+Kwa maana hivyo ndivyo ulivyoitayarisha dunia. 10  Unajaza maji katika mitaro yake na kusawazisha udongo wake uliolimwa;*Unailainisha kwa manyunyu ya mvua; unabariki mimea yake.+ 11  Unauvika mwaka taji kwa wema wako;Vijia vyako vinafurika kwa wingi wa vitu.*+ 12  Malisho ya nyikani yanaendelea kufurika,*+Na vilima vimevishwa shangwe.+ 13  Malisho yamefunikwa na makundi ya kondoo,Na mabonde yamefunikwa* na nafaka.+ Yanapaza sauti kwa ushindi, naam, yanaimba.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “watu wote wenye mwili.”
Au “Mahali pako patakatifu.”
Tnn., “ifurike.”
Au “matuta yake.”
Tnn., “vinadondosha mafuta.”
Tnn., “kudondosha.”
Au “nchi tambarare za chini zimefunikwa.”