Zaburi 66:1-20

  • Kazi za Mungu zinazostaajabisha

    • “Njooni mwone kazi za Mungu” (5)

    • “Nitatimiza nadhiri zangu kwako” (13)

    • Mungu husikia sala (18-20)

Kwa kiongozi. Wimbo. Muziki. 66  Mpazieni Mungu sauti ya ushindi, dunia yote.+   Liimbieni sifa* jina lake tukufu. Tukuzeni sifa yake.+   Mwambieni Mungu: “Kazi zako zinaogopesha kwelikweli!+ Kwa sababu ya nguvu zako nyingi,Maadui wako watajikunyata mbele zako.+   Dunia yote itakuinamia;+Watakuimbia sifa;Wataliimbia sifa jina lako.”+ (Sela)   Njooni mwone kazi za Mungu. Mambo aliyowatendea wanadamu yanaogopesha.+   Aliigeuza bahari kuwa nchi kavu;+Walivuka mto kwa miguu.+ Huko tulishangilia kwa sababu yake.+   Anatawala milele+ kwa nguvu zake. Macho yake yanachunguza mataifa.+ Wale ambao ni wakaidi hawapaswi kujikweza.+ (Sela)   Msifuni Mungu wetu, enyi mataifa,+Sauti ya sifa yake na isikiwe.   Yeye hutuhifadhi hai;*+Haruhusu miguu yetu ijikwae.*+ 10  Kwa maana umetuchunguza, Ee Mungu;+Umetusafisha kama fedha inavyosafishwa. 11  Ulituingiza katika wavu wa kuwindia;Ulitutwika mzigo mzito.* 12  Ulimruhusu mwanadamu anayeweza kufa apande juu yetu;*Tulipita motoni na katika maji;Kisha ukatuleta mahali penye kitulizo. 13  Nitaingia katika nyumba yako nikiwa na dhabihu nzima za kuteketezwa;+Nitatimiza nadhiri zangu kwako+ 14  Ambazo midomo yangu iliahidi+Na kinywa changu kilisema nilipokuwa katika taabu. 15  Nitakutolea dhabihu za kuteketezwa za wanyama waliononeshwaPamoja na moshi wa dhabihu za kondoo dume. Nitatoa ng’ombe dume pamoja na mbuzi dume. (Sela) 16  Njooni msikilize, ninyi nyote mnaomwogopa Mungu,Nami nitawaambia mambo aliyonitendea.+ 17  Nilimwita kwa kinywa changuNa kumtukuza kwa ulimi wangu. 18  Ikiwa nilihifadhi moyoni mwangu jambo lolote linalodhuru,Yehova hangenisikia.+ 19  Lakini Mungu alinisikia;+Aliisikiliza sala yangu.+ 20  Asifiwe Mungu, ambaye hakukataa sala yanguWala kuninyima upendo wake mshikamanifu.

Maelezo ya Chini

Au “Lipigieni muziki.”
Au “Hufanya nafsi zetu kuwa hai.”
Au “iyumbeyumbe; itetemeke.”
Tnn., “Uliweka mzigo mzito kwenye viuno vyetu.”
Tnn., “juu ya vichwa vyetu.”