Zaburi 67:1-7

  • Miisho ya dunia itamwogopa Mungu

    • Njia ya Mungu itajulikana (2)

    • ‘Mataifa yote na yamsifu Mungu’ (3, 5)

    • “Mungu atatubariki” (6, 7)

Kwa kiongozi; uimbwe kwa vinanda. Muziki. Wimbo. 67  Mungu atatuonyesha kibali na kutubariki;Atatuangazia nuru ya uso wake+ (Sela)   Ili njia yako ijulikane duniani kote,+Matendo yako ya wokovu miongoni mwa mataifa yote.+   Mataifa na yakusifu wewe, Ee Mungu;Mataifa yote na yakusifu.   Mataifa na yashangilie na kupaza sauti kwa shangwe,+Kwa maana utayahukumu mataifa kwa haki.+ Utayaongoza mataifa ya dunia. (Sela)   Mataifa na yakusifu, Ee Mungu;Mataifa yote na yakusifu wewe.   Dunia itatoa mazao yake;+Mungu, Mungu wetu, atatubariki.+   Mungu atatubariki,Na miisho yote ya dunia itamwogopa* yeye.+

Maelezo ya Chini

Au “itamheshimu.”