Zaburi 68:1-35

  • ‘Maadui wa Mungu na watawanyike’

    • “Baba wa mayatima” (5)

    • Mungu huwapa makao walio wapweke (6)

    • Wanawake wanatangaza habari njema (11)

    • Wanaume kuwa zawadi (18)

    • ‘Yehova hutubebea mzigo wetu kila siku’ (19)

Kwa kiongozi. Wa Daudi. Muziki. Wimbo. 68  Mungu na ainuke, maadui wake na watawanyike,Wale wanaomchukia na wakimbie kutoka mbele zake.+   Wapeperushe mbali kama moshi unavyopeperushwa;Kama nta inavyoyeyuka karibu na moto,Waovu na waangamie vivyo hivyo kutoka mbele za Mungu.+   Lakini waadilifu na washangilie;+Na wafurikwe na shangwe mbele za Mungu;Na wafurahi na kushangilia.   Mwimbieni Mungu; liimbieni sifa* jina lake.+ Mwimbieni Yule anayepanda kupitia jangwa tambarare.* Jina lake ni Yah!*+ Shangilieni mbele zake!   Baba wa mayatima na mlinzi* wa wajane+Ni Mungu katika makao yake matakatifu.+   Mungu huwapa makao walio peke yao;+Huwaachilia huru wafungwa na kuwafanikisha.+ Lakini ni lazima watu wakaidi* waishi katika nchi iliyokauka.+   Ee Mungu, ulipowaongoza* watu wako,+Ulipopiga mwendo jangwani, (Sela)   Dunia ilitetemeka;+Mbingu zilinyesha* mvua kwa sababu ya Mungu;Huu Mlima Sinai ulitetemeka kwa sababu ya Mungu, Mungu wa Israeli.+   Ulisababisha mvua kubwa inyeshe, Ee Mungu;Uliwatia nguvu tena watu wako waliochoka.* 10  Walikaa katika kambi yako yenye mahema;+Kwa wema wako, uliwaandalia maskini, Ee Mungu. 11  Yehova anatoa amri;Wanawake wanaotangaza habari njema ni jeshi kubwa.+ 12  Wafalme na majeshi yao wanakimbia,+ wanakimbia! Mwanamke anayebaki nyumbani anagawiwa nyara.+ 13  Ingawa ninyi wanaume mlikuwa mkilala katikati ya mioto kambini,*Kutakuwa na mabawa ya njiwa yaliyofunikwa kwa fedha,Yenye manyoya ya dhahabu bora.* 14  Mweza-Yote alipowatawanya wafalme waliokuwa nchini,+Theluji ilianguka Salmoni.* 15  Mlima wa Bashani+ ni mlima wa Mungu;*Mlima wa Bashani ni mlima wenye vilele. 16  Enyi milima yenye vilele, kwa nini mnautazama kwa wivu,Mlima ambao Mungu ameuchagua kuwa* makao yake?+ Kwa kweli, Yehova atakaa huko milele.+ 17  Magari ya Mungu ya vita ni makumi ya maelfu, maelfu kwa maelfu.+ Yehova ametoka Sinai na kuingia mahali patakatifu.+ 18  Ulipanda juu;+Ulichukua mateka;Ulichukua wanaume kuwa zawadi,+Naam, hata walio wakaidi,+ ili ukae miongoni mwao, Ee Yah Mungu. 19  Na asifiwe Yehova, anayetubebea mzigo wetu kila siku,+Mungu wa kweli wa wokovu wetu. (Sela) 20  Kwetu, Mungu wa kweli ni Mungu anayeokoa;+Na Yehova Bwana Mwenye Enzi Kuu huokoa kutoka katika kifo.+ 21  Naam, Mungu atapondaponda vichwa vya maadui wake,Utosi wenye nywele wa mtu yeyote anayeendelea kuwa na* hatia.+ 22  Yehova amesema: “Nitawarudisha kutoka Bashani;+Nitawarudisha kutoka katika vilindi vya bahari, 23  Ili mguu wako ufunikwe na damu+Na ulimi wa mbwa wako upate fungu lake kutoka kwa maadui.” 24  Wanaona misafara yako, Ee Mungu,Misafara ya Mungu wangu, Mfalme wangu, inayoingia mahali patakatifu.+ 25  Waimbaji wanatangulia mbele, wanamuziki wanaopiga vinanda wanawafuata;+Katikati yao kuna wanawake vijana wakipiga matari.+ 26  Katika umati uliokutanika,* msifuni Mungu;Msifuni Yehova, enyi mnaotoka katika Chemchemi ya Israeli.+ 27  Huko Benjamini,+ aliye mdogo zaidi, anawatiisha,Pia wakuu wa Yuda pamoja na umati wao wenye kelele,Wakuu wa Zabuloni, wakuu wa Naftali. 28  Mungu wako ameamuru kwamba utakuwa na nguvu. Onyesha nguvu zako, Ee Mungu, wewe ambaye umetenda kwa niaba yetu.+ 29  Kwa sababu ya hekalu lako lililo Yerusalemu,+Wafalme watakuletea zawadi.+ 30  Wakemee wanyama wa mwituni walio kwenye matete,Kusanyiko la ng’ombe dume+ na ndama wao,Mpaka mataifa yatakapoinama chini yakileta* vipande vya fedha. Lakini anayatawanya mataifa yanayopenda vita. 31  Vitu vya shaba nyekundu vitaletwa kutoka* Misri;+Kushi itafanya haraka kumpa Mungu zawadi. 32  Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,+Mwimbieni sifa* Yehova, (Sela) 33  Yule anayepanda mbingu ya kale kati ya mbingu.+ Tazama! Hunguruma kwa sauti yake, sauti yake yenye nguvu. 34  Tambueni nguvu za Mungu.+ Fahari yake iko juu ya Israeli,Na nguvu zake ziko angani.* 35  Mungu anaogopesha kutoka katika mahali pake patakatifu penye utukufu.+ Yeye ni Mungu wa Israeli,Anayewapa watu uwezo na nguvu.+ Asifiwe Mungu.

Maelezo ya Chini

Au “lipigieni muziki.”
Au labda, “juu ya mawingu.”
“Yah” ni ufupisho wa jina Yehova.
Tnn., “mwamuzi.”
Au “waasi.”
Tnn., “ulipotangulia mbele ya.”
Tnn., “zilidondosha.”
Tnn., “Uliutia nguvu tena urithi wako.”
Au labda, “katikati ya mazizi ya kondoo.”
Au “yenye mchanganyiko wa rangi ya manjano na kijani kibichi.”
Au “Ni kana kwamba theluji ilianguka Salmoni.”
Au “ni mlima mrefu.”
Au “anatamani uwe.”
Au “anayetembeatembea katika.”
Tnn., “Katika makusanyiko.”
Au labda, “yakikanyagia chini.”
Au labda, “Mabalozi watatoka.”
Au “Mpigieni muziki.”
Tnn., “mawinguni.”