Zaburi 7:1-17

  • Yehova ni Mwamuzi mwadilifu

    • “Nihukumu, Ee Yehova” (8)

Wimbo wa huzuni* wa Daudi ambao alimwimbia Yehova kwa sababu ya maneno ya Kushi Mbenjamini. 7  Ee Yehova Mungu wangu, nimekukimbilia wewe.+ Niokoe kutoka kwa wale wote wanaonitesa na unifanye nisalimike.+   La sivyo watanirarua* vipandevipande kama simba anavyofanya,+Watanibeba na kwenda nami pasipo na yeyote wa kuniokoa.   Ee Yehova Mungu wangu, ikiwa nimekosea katika jambo hili,Ikiwa nimetenda isivyo haki,   Ikiwa nimemkosea anayenitendea wema,+Au ikiwa nimempora adui yangu bila sababu,*   Basi acha adui anikimbize na kunipita;*Acha aukanyagie uhai wangu ardhiniNa kuufanya utukufu wangu utokomee mavumbini. (Sela)   Inuka katika hasira yako, Ee Yehova;Simama ukabiliane na hasira kali ya maadui wangu;+Amka kwa ajili yangu, na uamuru kwamba haki itendeke.+   Acha mataifa yakuzingire;Nawe utachukua hatua dhidi yao kutoka juu.   Yehova atayahukumu mataifa.+ Nihukumu, Ee Yehova, kulingana na uadilifu wanguNa kulingana na utimilifu wangu.+   Tafadhali, yakomeshe matendo maovu ya waovu. Lakini umwimarishe mwadilifu,+Kwa kuwa wewe ni Mungu mwadilifu+ anayechunguza mioyo+ na hisia zilizo ndani kabisa.*+ 10  Mungu ni ngao yangu,+ Mwokozi wa wale walio wanyoofu moyoni.+ 11  Mungu ni Mwamuzi mwadilifu,+Na Mungu huzitangaza hukumu zake* kila siku. 12  Mtu yeyote asipotubu,+ Yeye huunoa upanga wake;+Huukunja upinde wake na kuuweka tayari.+ 13  Hutayarisha silaha zake zinazoua;Huweka tayari mishale yake inayowaka moto.+ 14  Mtazame yule aliye na mimba ya uovu;Hutunga mimba ya matatizo na kuzaa uwongo.+ 15  Huchimba shimo na kuzidisha kina chake,Lakini huanguka katika shimo hilohilo alilolichimba.+ 16  Matatizo anayosababisha yatarudi juu ya kichwa chake mwenyewe;+Ukatili wake utaanguka juu ya utosi wa kichwa chake. 17  Nitamsifu Yehova kwa sababu ya haki yake;+Nitaliimbia sifa* jina la Yehova+ Aliye Juu Zaidi.+

Maelezo ya Chini

Au “Wimbo wa maombolezo.
Au “watairarua nafsi yangu.”
Au labda, “Nilipomwacha hai yule anayenipinga bila sababu.”
Au “na kuipita nafsi yangu.”
Au “anayejaribu mioyo na figo.”
Au “huvurumisha shutuma zake.”
Au “Nitalipigia muziki.”