Zaburi 70:1-5

  • Aomba asaidiwe haraka

    • “Tenda haraka kwa niaba yangu” (5)

Kwa kiongozi. Wa Daudi, wa kukumbusha. 70  Ee Mungu, niokoe;Ee Yehova, njoo haraka unisaidie.+   Wale wanaotaka kuniua*Na waaibishwe na kufedheheshwa. Wale wanaofurahia msiba wanguNa wakimbie kwa aibu.   Wale wanaosema: “Aha! Aha!” Na wakimbizwe kwa aibu.   Lakini acha wale wanaokutafutaWafurahi na kushangilia kwa sababu yako.+ Wale wanaopenda matendo yako ya wokovu na waseme daima: “Mungu na atukuzwe!”   Lakini sina uwezo, nami ni maskini;+Ee Mungu, tenda haraka kwa niaba yangu.+ Wewe ni msaidizi wangu na mwokozi wangu.+ Ee Yehova, usikawie.+

Maelezo ya Chini

Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”