Zaburi 71:1-24

  • Tegemeo la waliozeeka

    • Kumtumaini Mungu tangu wakati wa ujana (5)

    • “Ninapoishiwa na nguvu” (9)

    • ‘Mungu amenifundisha tangu nilipokuwa kijana’ (17)

71  Nimekukimbilia wewe, Ee Yehova. Usiache niaibishwe kamwe.+   Niokoe na kuninusuru kwa uadilifu wako. Nitegee sikio lako* na uniokoe.+   Uwe ngome ya mwamba kwanguAmbamo ninaweza kuingia sikuzote. Toa amri ya kuniokoa,Kwa maana wewe ni jabali langu na ngome yangu.+   Ee Mungu wangu, niokoe kutoka mikononi mwa mwovu,+Kutoka katika makucha ya mkandamizaji asiyetenda haki.   Kwa maana wewe ni tumaini langu, Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova;Nimekutumaini wewe* tangu nilipokuwa kijana.+   Nimekutegemea tangu nilipozaliwa;Wewe ndiye uliyenitoa tumboni mwa mama yangu.+ Ninakusifu daima.   Nimekuwa kama muujiza kwa watu wengi,Lakini wewe ni kimbilio langu imara.   Kinywa changu kimejaa sifa zako;+Mchana kutwa ninasimulia kuhusu fahari yako.   Usinitupe wakati wa uzee;+Usiniache ninapoishiwa na nguvu.+ 10  Maadui wangu wanasema mambo mabaya kunihusu,Na wale wanaotaka kuniua* wanapanga njama pamoja,+ 11  Wakisema: “Mungu amemwacha. Mkimbizeni na kumkamata, kwa maana hakuna yeyote wa kumwokoa.”+ 12  Ee Mungu, usiendelee kukaa mbali nami. Ee Mungu wangu, njoo haraka unisaidie.+ 13  Wale wanaonipingaNa waaibishwe na kuangamia.+ Wale wanaonitakia msibaNa wafunikwe na aibu na fedheha.+ 14  Lakini mimi, nitaendelea kungoja;Nitakusifu hata zaidi. 15  Kinywa changu kitasimulia uadilifu wako,+Mchana kutwa kitasimulia matendo yako ya wokovu,Ingawa ni mengi sana kwangu kuyajua.*+ 16  Nitakuja na kutangaza matendo yako yenye nguvu,Ee Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova;Nitatangaza uadilifu wako, wako peke yako. 17  Ee Mungu, umenifundisha tangu nilipokuwa kijana,+Na mpaka sasa ninaendelea kutangaza kazi zako zinazostaajabisha.+ 18  Ee Mungu, hata nikizeeka na kuwa na mvi, usiniache.+ Acha nikiambie kizazi kijacho kuhusu nguvu zako*Na kuwaambia wote watakaokuja kuhusu uwezo wako.+ 19  Uadilifu wako, Ee Mungu, unafika vileleni;+Umetenda mambo makuu;Ee Mungu, ni nani aliye kama wewe?+ 20  Ingawa umenifanya nipate taabu nyingi na misiba mingi,+Nihuishe tena;Niinue kutoka katika sehemu zenye kina za* dunia.+ 21  Ongeza ukuu wanguNizunguke na kunifariji. 22  Kisha nitakusifu kwa zezeKwa sababu ya uaminifu wako, Ee Mungu wangu.+ Nitaimba sifa zako* kwa kinubi,Ee Mtakatifu wa Israeli. 23  Midomo yangu itapaza sauti kwa shangwe ninapokuimbia sifa,+Kwa maana umeokoa uhai wangu.*+ 24  Ulimi wangu utaongea* kuhusu uadilifu wako mchana kutwa,+Kwa maana wale wanaotaka kuniangamiza wataaibishwa na kufedheheshwa.+

Maelezo ya Chini

Au “Inama chini na unisikilize.”
Au “Wewe ni tegemeo langu.”
Au “wanaoitafuta nafsi yangu.”
Au “kuyahesabu.”
Tnn., “mkono wako.”
Au “vilindi vya.”
Au “Nitakupigia muziki.”
Au “umeikomboa nafsi yangu.”
Au “utatafakari.”