Zaburi 72:1-20

  • Utawala wa amani wa mfalme aliyewekwa na Mungu

    • “Mwadilifu atasitawi” (7)

    • Raia kutoka bahari mpaka bahari (8)

    • Kuokolewa kutoka katika ukatili (14)

    • Nafaka itakuwa nyingi duniani (16)

    • Jina la Mungu lasifiwa milele (19)

Zaburi Inayomhusu Sulemani. 72  Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako,Na umzawadie mwana wa mfalme uadilifu wako.+   Na atetee kesi ya watu wako kwa uadilifu,Na ya watu wako wa hali ya chini kwa haki.+   Milima na iwaletee watu amani,Na vilima vilete uadilifu.   Na awalinde* watu wa hali ya chini miongoni mwa mataifa,Na awaokoe watoto* wa mtu maskini,Na amponde mpunjaji.+   Watakuogopa maadamu jua lipoNa maadamu mwezi unadumu,Kizazi baada ya kizazi.+   Atakuwa kama mvua inayonyeshea majani yaliyofyekwa,Kama manyunyu ya mvua yanayoinywesha dunia.+   Katika siku zake mwadilifu atasitawi,*+Na amani itakuwa nyingi+ mpaka mwezi utakapokuwa haupo tena.   Atakuwa na raia* kutoka bahari mpaka bahariNa kutoka Mto Efrati mpaka kwenye miisho ya dunia.+   Wakaaji wa jangwani watainama chini mbele yake,Na maadui wake wataramba mavumbi.+ 10  Wafalme wa Tarshishi na wa visiwa watalipa ushuru.+ Wafalme wa Sheba na wa Seba watatoa zawadi.+ 11  Wafalme wote watainama chini mbele yake,Na mataifa yote yatamtumikia. 12  Kwa maana atamwokoa maskini anayelilia msaada,Pia mtu wa hali ya chini na yeyote ambaye hana msaidizi. 13  Atamhurumia mtu wa hali ya chini na maskini,Naye ataokoa uhai wa* maskini. 14  Atawaokoa* kutoka katika ukandamizaji na ukatili,Na damu yao itakuwa na thamani machoni pake. 15  Na aishi na kupewa dhahabu ya Sheba.+ Sala na zitolewe daima kwa ajili yake,Na abarikiwe mchana kutwa. 16  Kutakuwa na nafaka nyingi duniani;+Itafurika juu ya milima. Matunda yake yatasitawi kama ya Lebanoni,+Na katika majiji watu watachanua kama mimea ya dunia.+ 17  Jina lake na lidumu milele,+Na lisitawi maadamu jua lipo. Watu na wajipatie baraka kupitia yeye;+Mataifa yote na yamtangaze kuwa mwenye furaha. 18  Na asifiwe Yehova Mungu, Mungu wa Israeli,+Ambaye peke yake hutenda mambo yanayostaajabisha.+ 19  Jina lake tukufu na lisifiwe milele,+Na utukufu wake ujae duniani pote.+ Amina na Amina. 20  Huo ndio mwisho wa sala za Daudi, mwana wa Yese.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “awahukumu.”
Au “wana.”
Tnn., “atachipuka.”
Au “Atatawala.”
Au “nafsi za.”
Au “Atazikomboa nafsi zao.”