Zaburi 73:1-28

  • Mtu aliyemwogopa Mungu arudiwa na ufahamu wa kiroho

    • “Hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza” (2)

    • “Nilitaabika mchana kutwa” (14)

    • “Mpaka nilipoingia mahali patakatifu pa Mungu” (17)

    • Waovu wako kwenye ardhi yenye utelezi (18)

    • Kumkaribia Mungu ni jambo jema (28)

Muziki wa Asafu.+ 73  Kwa kweli Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale walio safi moyoni.+   Lakini mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kukengeuka;Hatua zangu zilikuwa karibu kuteleza.+   Kwa maana niliwaonea wivu wenye kiburi*Nilipokuwa nikiona amani ya waovu.+   Kwa maana hawana maumivu wanapokufa;Miili yao ina afya.*+   Hawataabiki kama wanadamu wengine,+Wala hawateseki kama watu wengine.+   Kwa hiyo, kiburi ni mkufu wao;+Ukatili huwafunika kama vazi.   Ufanisi wao* hufanya macho yao yanenepe;Wamezidi mawazo ya moyo.   Wanadhihaki na kusema mambo maovu.+ Kwa kiburi, wanatoa vitisho vya kuwakandamiza wengine.+   Wanaongea kana kwamba wako juu kama mbingu,Na ndimi zao hutamba duniani. 10  Kwa hiyo watu wake huwageukia,Nao hunywa maji yao mengi. 11  Wanasema: “Mungu anajuaje?+ Je, Aliye Juu Zaidi ana ujuzi kweli?” 12  Naam, hivyo ndivyo walivyo waovu, ambao sikuzote wanastarehe.+ Wanaendelea kuongeza mali zao.+ 13  Kwa hakika nimeusafisha moyo wangu bureNa kunawa mikono yangu katika ukosefu wa hatia.+ 14  Nami nilitaabika mchana kutwa;+Niliadhibiwa kila asubuhi.+ 15  Lakini kama ningesema mambo hayo,Ningewasaliti watu wako.* 16  Nilipojaribu kulielewa jambo hilo,Lilinitaabisha 17  Mpaka nilipoingia mahali patakatifu pa Mungu penye utukufu,Nami nikatambua wakati wao ujao. 18  Kwa hakika unawaweka kwenye ardhi yenye utelezi.+ Unawafanya waanguke katika uharibifu wao.+ 19  Jinsi wanavyoangamizwa kwa ghafla!+ Jinsi wanavyofikia kwa ghafla mwisho wao unaotisha! 20  Kama ndoto wakati wa kuamka, Ee Yehova,Utakapoinuka, utaitupilia mbali* sanamu yao. 21  Lakini moyo wangu ulikuwa mchungu,+Na ndani kabisa* nilihisi maumivu makali. 22  Nilikuwa mpumbavu wala sikuwa na uelewaji;Nilikuwa kama mnyama asiye na akili mbele zako. 23  Lakini sasa niko pamoja nawe sikuzote;Umeushika mkono wangu wa kulia.+ 24  Unaniongoza kwa ushauri wako,+Na baadaye utaniongoza kwenye utukufu.+ 25  Ni nani niliye naye mbinguni? Isipokuwa wewe tu, sitamani chochote duniani.+ 26  Mwili wangu na moyo wangu unaweza kudhoofika,Lakini Mungu ni mwamba wa moyo wangu na fungu langu milele.+ 27  Kwa kweli, wale wanaojitenga mbali nawe wataangamia. Utamwangamiza* kila mtu anayekuacha kwa upotovu.*+ 28  Lakini kwa upande wangu, kumkaribia Mungu ni jambo jema kwangu.+ Nimemfanya Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova kuwa kimbilio langu,Ili nizitangaze kazi zako zote.+

Maelezo ya Chini

Au “wanaojigamba.”
Au “Kitambi chao kimenenepa.”
Tnn., “Mafuta yao.”
Tnn., “Ningekisaliti kizazi cha wana wako.”
Tnn., “utaidharau.”
Tnn., “katika figo zangu.”
Tnn., “Utamnyamazisha.”
Au “kukosa uaminifu.”