Zaburi 75:1-10

  • Mungu ahukumu kwa haki

    • Waovu watakunywa kikombe cha Yehova (8)

Kwa kiongozi. Umepatanishwa na muziki wa “Usiharibu.” Wimbo wa Asafu.+ 75  Tunakushukuru, Ee Mungu, tunakushukuru;Jina lako liko karibu,+Na watu wanatangaza kazi zako zinazostaajabisha.   Unasema: “Ninapoweka wakati hususa,Ninahukumu kwa haki.   Dunia na wakaaji wake wote walipoyeyushwa,Mimi ndiye niliyeziimarisha nguzo zake.” (Sela)   Ninawaambia wenye kujigamba, “Msijigambe,” Na waovu, “Msikweze nguvu zenu.*   Msikweze nguvu zenu* juu sanaAu kuongea kwa kiburi.   Kwa maana kukwezwaHakutoki mashariki wala magharibi wala kusini.   Kwa maana Mungu ni Mwamuzi.+ Humshusha huyu na kumkweza yule.+   Kwa maana kuna kikombe mkononi mwa Yehova;+Divai inatoa povu nayo imechanganywa kikamili. Hakika ataimwaga,Na waovu wote duniani watainywa, mpaka machicha yake.”+   Lakini mimi, nitalitangaza hilo milele;Nitamwimbia sifa* Mungu wa Yakobo. 10  Kwa maana anasema: “Nitazikata nguvu* zote za waovu.” Lakini nguvu* za waadilifu zitakwezwa.

Maelezo ya Chini

Tnn., “pembe yenu.”
Tnn., “pembe yenu.”
Au “Nitampigia muziki.”
Tnn., “pembe.”
Tnn., “pembe.”