Zaburi 76:1-12

  • Mungu atawashinda maadui wa Sayuni

    • Mungu awaokoa wapole (9)

    • Maadui wenye kiburi watanyenyekezwa (12)

Kwa kiongozi; uimbwe kwa ala za nyuzi. Muziki wa Asafu.+ Wimbo. 76  Mungu anajulikana Yuda;+Jina lake ni kuu katika Israeli.+   Banda lake liko Salemu,+Na makao yake yako Sayuni.+   Huko aliivunja mishale inayowaka ya upinde,Ngao na upanga na silaha za vita.+ (Sela)   Unang’aa kwa uangavu;*Una fahari kuliko milima ya mawindo.   Wenye moyo jasiri wameporwa.+ Wamelala usingizi;Mashujaa wote hawakuwa na uwezo.+   Kwa sababu ya kemeo lako, Ee Mungu wa Yakobo,Mwendeshaji wa gari na farasi wote wamelala usingizi mzito.+   Ni wewe peke yako unayeogopesha.+ Na ni nani anayeweza kustahimili hasira yako kali?+   Kutoka mbinguni ulitangaza hukumu;+Dunia iliogopa na kunyamaza+   Mungu alipoinuka ili kutekeleza hukumu,Ili kuwaokoa wapole wote walio duniani.+ (Sela) 10  Kwa maana ghadhabu ya mwanadamu itakuletea sifa;+Nawe utajipamba kwa mabaki ya ghadhabu yao. 11  Wekeni nadhiri zenu kwa Yehova Mungu wenu na kuzitimiza,+Wote wanaomzunguka na walete zawadi yao kwa woga.+ 12  Atakinyenyekeza kiburi cha* viongozi;Yeye huwaogopesha wafalme wa dunia.

Maelezo ya Chini

Au “Umefunikwa na nuru.”
Tnn., “Atainyenyekeza roho ya.”