Zaburi 78:1-72

  • Utunzaji wa Mungu na ukosefu wa imani wa Waisraeli

    • Kisimulie kizazi kijacho (2-8)

    • “Hawakudhihirisha imani katika Mungu” (22)

    • “Nafaka ya mbinguni” (24)

    • “Wakamhuzunisha Mtakatifu wa Israeli” (41)

    • Kutoka Misri mpaka Nchi ya Ahadi (43-55)

    • “Waliendelea kumjaribu Mungu” (56)

Maskili.* Wa Asafu.+ 78  Sikilizeni sheria* yangu, enyi watu wangu;Tegeni sikio lenu kwa maneno ya kinywa changu.   Nitakifungua kinywa changu kwa methali. Nitafumbua mafumbo ya zamani za kale.+   Mambo ambayo tumesikia na tunayojua,Ambayo baba zetu wametusimulia,+   Hatutawaficha wana wao;Tutakisimulia kizazi kijacho mambo hayo+Matendo ya Yehova yanayostahili sifa na nguvu zake,+Mambo yanayostaajabisha aliyotenda.+   Alianzisha kikumbusho katika YakoboNa kuweka sheria katika Israeli;Aliwaamuru mababu zetuWawajulishe watoto wao mambo hayo,+   Ili kizazi kijacho,Watoto ambao hawajazaliwa, wayajue.+ Kisha wao watawasimulia watoto wao.+   Halafu watoto hao watamtumaini Mungu. Hawatasahau kazi za Mungu+Lakini watashika amri zake.+   Kisha hawatakuwa kama mababu zao,Kizazi chenye ukaidi na uasi,+Kizazi kilichokuwa na moyo unaoyumbayumba*+Na ambacho hakikuwa na roho ya uaminifu kwa Mungu.   Waefraimu walijihami kwa upinde,Lakini walikimbia siku ya vita. 10  Hawakushika agano la Mungu+Nao walikataa kutembea katika sheria yake.+ 11  Walisahau pia mambo aliyotenda,+Kazi zake zinazostaajabisha alizowaonyesha.+ 12  Alifanya maajabu mbele ya mababu zao,+Katika nchi ya Misri, eneo la Soani.+ 13  Aliipasua bahari ili kuwaruhusu wavuke,Naye akayafanya maji yasimame juu kama bwawa.*+ 14  Aliwaongoza kwa wingu wakati wa mchanaNa usiku kucha kwa mwangaza wa moto.+ 15  Aliipasua miamba nyikani,Akawanywesha maji ya kutosha kana kwamba yanatoka vilindini.+ 16  Alivitoa vijito kutoka kwenye jabaliNa kufanya maji yatiririke chini kama mito.+ 17  Lakini waliendelea kumtendea dhambiKwa kumwasi jangwani yule Aliye Juu Zaidi;+ 18  Walimjaribu* Mungu moyoni mwao+Walidai wapewe chakula walichotamani.* 19  Kwa hiyo wakalalamika kumhusu Mungu,Wakisema: “Je, Mungu anaweza kuandaa meza nyikani?”+ 20  Tazama! Aliupiga mwambaHivi kwamba maji yakatiririka na vijito vikafurika.+ “Je, anaweza pia kutupatia mkate,Au je, anaweza kuwapa watu wake nyama?”+ 21  Yehova alipowasikia, alikasirika sana;+Moto+ ukawaka dhidi ya Yakobo,Na hasira yake ikawaka dhidi ya Israeli+ 22  Kwa sababu hawakudhihirisha imani katika Mungu;+Hawakuutumaini uwezo wake wa kuwaokoa. 23  Basi akaliamuru anga lililo juu lenye mawingu,Naye akaifungua milango ya mbingu. 24  Akaendelea kuwanyeshea mana ili wale;Akawapa nafaka ya mbinguni.+ 25  Wanadamu wakala mkate wa wenye nguvu;*+Aliwapa mkate wa kutosha wa kuwashibisha.+ 26  Aliuvumisha upepo wa mashariki mbinguniNa kwa nguvu zake akaufanya upepo wa kusini uvume.+ 27  Naye akawanyeshea nyama kama mavumbi,Ndege kama mchanga kwenye ufuo wa bahari. 28  Aliwaangusha katikati ya kambi yake,Pande zote kuzunguka mahema yake. 29  Nao wakala na kujilazimisha kula zaidi;Aliwapa walichotamani.+ 30  Lakini kabla hawajatosheleza kikamili tamaa yao,Chakula kilipokuwa kingali kinywani mwao, 31  Ghadhabu ya Mungu ikawaka dhidi yao.+ Akawaua wanaume wenye nguvu zaidi;+Aliwaangamiza wanaume vijana wa Israeli. 32  Licha ya hayo walizidi kutenda dhambi+Nao hawakudhihirisha imani katika kazi zake zinazostaajabisha.+ 33  Basi akazikatisha siku zao kana kwamba ni pumzi tu,+Na miaka yao kwa matukio ya ghafla yenye kutisha. 34  Lakini kila mara alipowaua baadhi yao, waliosalia walimtafuta;+Walirudi na kumtafuta Mungu, 35  Wakikumbuka kwamba Mungu alikuwa Mwamba wao+Na kwamba Mungu Aliye Juu Zaidi alikuwa Mkombozi* wao.+ 36  Lakini walijaribu kumdanganya kwa kinywa chaoNa kumwambia uwongo kwa ulimi wao. 37  Moyo wao haukuwa imara kumwelekea;+Nao hawakuwa waaminifu kwa agano lake.+ 38  Lakini alikuwa mwenye rehema;+Alikuwa akiwasamehe* kosa lao, naye hakuwaangamiza.+ Mara nyingi aliizuia hasira yake+Badala ya kuichochea ghadhabu yake yote. 39  Kwa maana alikumbuka kwamba walikuwa nyama tu,+Upepo upitao ambao haurudi.* 40  Jinsi walivyomwasi mara nyingi nyikani+Na kumtia uchungu jangwani!+ 41  Walimjaribu Mungu tena na tena,+Nao wakamhuzunisha* Mtakatifu wa Israeli. 42  Hawakuzikumbuka nguvu zake,*Siku ambayo aliwaokoa* kutoka kwa adui,+ 43  Jinsi alivyoonyesha ishara zake kule Misri+Na miujiza yake katika eneo la Soani, 44  Na jinsi alivyobadili mifereji ya Nile kuwa damu+Hivi kwamba hawangeweza kunywa maji kutoka katika vijito vyake. 45  Alituma makundi ya nzi ili yawale+Na vyura ili kuwaangamiza.+ 46  Mazao yao aliwapa parare wanaokula sana,Matunda ya kazi yao ngumu akayapa makundi ya nzige.+ 47  Aliharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe+Na mikuyu yao kwa mawe ya mvua. 48  Aliwaua kwa mvua ya mawe wanyama wao wa kubeba mizigo+Na mifugo yao kwa umeme wa radi.* 49  Aliwamwagia hasira yake inayowaka,Hasira kali na ghadhabu na taabu,Makundi ya malaika yanayoleta msiba. 50  Alitayarisha njia kwa ajili ya hasira yake. Hakuwalinda wasife;*Naye aliwaua kwa ugonjwa hatari. 51  Mwishowe aliwaangamiza wazaliwa wote wa kwanza wa Misri,+Mwanzo wa nguvu zao za uzazi katika mahema ya Hamu. 52  Kisha akawatoa nje watu wake kama kundi la kondoo+Na kuwaongoza nyikani kama kundi la mifugo. 53  Aliwaongoza kwa usalama,Nao hawakuogopa;+Bahari iliwafunika maadui wao.+ 54  Naye akawaleta katika eneo lake takatifu,+Eneo hili lenye milima ambalo mkono wake wa kuume ulilitwaa.+ 55  Aliyafukuza mataifa kutoka mbele yao;+Akawagawia urithi kwa kamba ya kupimia;+Aliyafanya makabila ya Israeli yakae katika makao yao.+ 56  Lakini waliendelea kumjaribu* Mungu Aliye Juu Zaidi, na kumwasi;+Hawakusikiliza vikumbusho vyake.+ 57  Pia walipotoka na kutenda kwa hila kama mababu zao.+ Hawakutegemeka kama upinde uliolegea usivyotegemeka.+ 58  Waliendelea kumkasirisha kwa mahali pao pa juu,+Nao wakachochea hasira yake kali* kwa sanamu zao za kuchongwa.+ 59  Mungu alisikia na kuwaka hasira,+Kwa hiyo akaikataa kabisa Israeli. 60  Mwishowe akaliacha hema la ibada lililo Shilo,+Hema alimokaa miongoni mwa wanadamu.+ 61  Aliacha ishara ya nguvu zake ipelekwe utekwani;Fahari yake itiwe mikononi mwa adui.+ 62  Aliwatoa watu wake wauawe kwa upanga+Naye akaukasirikia vikali urithi wake. 63  Moto uliwateketeza kabisa vijana wake wa kiume,Na mabikira wake hawakuimbiwa nyimbo za harusi.* 64  Makuhani wake waliuawa kwa upanga,+Na wajane wao hawakulia.+ 65  Kisha Yehova akaamka kana kwamba anatoka usingizini,+Kama mwanamume hodari+ aamkavyo baada ya divai kumtoka. 66  Naye akawakimbiza maadui wake;+Akawatia aibu ya kudumu. 67  Alilikataa hema la Yosefu;Hakulichagua kabila la Efraimu. 68  Lakini alichagua kabila la Yuda,+Mlima Sayuni, anaoupenda.+ 69  Alipafanya mahali pake patakatifu pawe mahali pa kudumu kama mbingu,*+Kama dunia ambayo ameiimarisha milele.+ 70  Alimchagua Daudi+ mtumishi wakeNa kumtoa katika mazizi ya kondoo,+ 71  Alimwondoa katika kazi ya kuchunga kondoo wanaonyonyesha;Akamfanya kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake,+Na wa Israeli, urithi wake.+ 72  Aliwachunga kwa utimilifu wa moyo,+Na kwa mikono stadi aliwaongoza.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “mafundisho.”
Tnn., “ambao haujatayarishwa.”
Au “ukuta.”
Tnn., “Walimtahini.”
Au “chakula kwa ajili ya nafsi yao.”
Au “wa malaika.”
Au “Mlipiza-Kisasi.”
Tnn., “akifunika.”
Au labda, “Kwamba roho inaenda nayo hairudi.”
Au “wakamtia uchungu.”
Tnn., “Hawakuukumbuka mkono wake.”
Tnn., “aliwakomboa.”
Au labda, “homa kali.”
Au “Hakulinda nafsi zao zisife.”
Tnn., “kumtahini.”
Au “wivu wake.”
Tnn., “hawakusifiwa.”
Tnn., “Alipajenga mahali pake patakatifu kama vilele.”