Zaburi 79:1-13

  • Sala iliyotolewa mataifa yalipowavamia watu wa Mungu

    • ‘Sisi ni kitu cha kushutumiwa’ (4)

    • ‘Tusaidie kwa ajili ya jina lako’ (9)

    • “Walipize jirani zetu mara saba” (12)

Muziki wa Asafu.+ 79  Ee Mungu, mataifa yamevamia urithi wako;+Yamelichafua hekalu lako takatifu;+Yamebadili Yerusalemu kuwa rundo la magofu.+   Wamewapa ndege wa angani maiti za watumishi wako kuwa chakula chaoNa miili ya washikamanifu wako wamewapa wanyama wa mwituni wa dunia.+   Wamemwaga damu yao kama maji kotekote Yerusalemu,Na hakuna aliyebaki wa kuwazika.+   Tumekuwa kitu cha kushutumiwa na majirani wetu;+Wale wanaotuzunguka wanatudhihaki na kutufanyia mzaha.   Ee Yehova, utaendelea kuwaka hasira mpaka lini? Milele?+ Ghadhabu yako itaendelea kuwaka kama moto mpaka lini?+   Yamwagie ghadhabu yako mataifa ambayo hayakujuiNa falme ambazo haziliitii jina lako.+   Kwa maana wamemnyafua YakoboNao wameifanya nchi yake ukiwa.+   Usitufanye tuwajibike kwa sababu ya makosa ya mababu zetu.+ Tuonyeshe haraka rehema yako,+Kwa maana tumeshushwa chini sana.   Tusaidie, Ee Mungu wa wokovu wetu,+Kwa ajili ya jina lako tukufu;Tuokoe na kutusamehe* dhambi zetu kwa ajili ya jina lako.+ 10  Kwa nini mataifa yaseme: “Mungu wao yuko wapi?”+ Na ijulikane miongoni mwa mataifa mbele ya macho yetuKwamba damu iliyomwagwa ya watumishi wako imelipiziwa kisasi.+ 11  Na usikie kilio cha maumivu cha mfungwa.+ Tumia nguvu zako kuu* kuwahifadhi* wale waliohukumiwa kifo.*+ 12  Walipize majirani wetu mara saba+Kwa sababu ya shutuma walizotoa dhidi yako, Ee Yehova.+ 13  Kisha sisi, watu wako na kondoo wa malisho yako,+Tutakushukuru milele;Nasi tutatangaza sifa yako kizazi mpaka kizazi.+

Maelezo ya Chini

Tnn., “ufunike.”
Tnn., “mkono wako.”
Au labda, “kuwaweka huru.”
Tnn., “wana wa kifo.”