Zaburi 8:1-9

  • Utukufu wa Mungu na heshima ya mwanadamu

    • “Jinsi jina lako lilivyo kuu!” (1, 9)

    • ‘Mwanadamu anayeweza kufa ana faida gani?’ (4)

    • Mwanadamu avikwa taji la fahari (5)

Kwa kiongozi; juu ya Gitithi.* Muziki wa Daudi. 8  Ee Yehova Bwana wetu, jinsi jina lako lilivyo kuu katika dunia yote;Umeweka fahari yako juu zaidi hata kuliko mbingu!*+   Kutoka katika vinywa vya watoto wadogo na wanaonyonya+ umeimarisha nguvuKwa sababu ya maadui wako,Ili kumnyamazisha adui na yule anayelipiza kisasi.   Ninapoziona mbingu zako, kazi za vidole vyako,Mwezi na nyota ambazo umetayarisha,+   Mwanadamu anayeweza kufa ni nini hivi kwamba unamweka akilini,Na mwana wa mtu hivi kwamba unamtunza?+   Ulimfanya awe mdogo kidogo kuliko wale walio kama Mungu,*Nawe ukamvika taji la utukufu na fahari.   Ulimpa mamlaka juu ya kazi za mikono yako;+Umeweka kila kitu chini ya miguu yake:   Kondoo wote na ng’ombe wote,Na pia wanyama wa mwituni,+   Ndege wa angani na samaki wa baharini,Kitu chochote kinachopita katika njia za baharini.   Ee Yehova Bwana wetu, jinsi jina lako lilivyo kuu katika dunia yote!

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au labda, “Wewe ambaye fahari yako inasimuliwa juu ya mbingu!”
Au “kuliko malaika.”