Zaburi 80:1-19

  • Mchungaji wa Israeli atafutwa ili awarudishe

    • “Ee Mungu, turudishe” (3)

    • Israeli, mzabibu wa Mungu (8-15)

Kwa kiongozi; umepatanishwa na mtindo wa “Mayungiyungi.” Kikumbusho. Muziki wa Asafu.+ 80  Ee Mchungaji wa Israeli, sikiliza,Wewe unayemwongoza Yosefu kama kundi la kondoo.+ Wewe unayeketi kwenye kiti cha ufalme juu ya* makerubi,+Angaza.*   Mbele ya Efraimu na Benjamini na Manase,Chochea nguvu zako;+Njoo utuokoe.+   Ee Mungu, turudishe;+Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+   Yehova Mungu wa majeshi, utaendelea mpaka lini kuwa na hasira kali kuelekea* sala ya watu wako?+   Unawalisha machozi kama mkate,Nawe unawanywesha machozi kupita kiasi.   Unawaruhusu majirani wetu wagombane kwa sababu yetu;Maadui wetu wanaendelea kutudhihaki wapendavyo.+   Ee Mungu wa majeshi, turudishe;Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+   Uliufanya mzabibu+ uondoke Misri. Uliyafukuza mataifa na kuupanda.+   Ulitayarisha nafasi kwa ajili yake,Nao ukatia mizizi na kujaa nchini.+ 10  Milima ilifunikwa kwa kivuli chake,Na mierezi ya Mungu kwa matawi yake. 11  Matawi yake yalienea mpaka baharini,Na machipukizi yake mpaka kwenye Mto Efrati.+ 12  Kwa nini umebomoa kuta za mawe za shamba la mzabibu huo,+Hivi kwamba wote wanaopita karibu nao wanachuma matunda yake?+ 13  Nguruwe wa mwituni wanauharibu,Na wanyama wa porini wanaula.+ 14  Ee Mungu wa majeshi, rudi tafadhali. Tazama chini kutoka mbinguni uone! Utunze mzabibu huu,+ 15  Shina* ambalo mkono wako wa kuume umepanda,+Na umtazame mwana ambaye umemtia nguvu* kwa ajili yako mwenyewe.+ 16  Umechomwa moto,+ umekatwa. Wanaangamia kwa kemeo lako.* 17  Mkono wako na umtegemeze mwanamume aliye kwenye mkono wako wa kuume,Mwana wa binadamu uliyemtia nguvu kwa ajili yako mwenyewe.+ 18  Kisha hatutageuka kutoka kwako. Tuhifadhi hai, ili tuliitie jina lako. 19  Ee Yehova Mungu wa majeshi, turudishe;Uso wako na utuangazie, ili tuokolewe.+

Maelezo ya Chini

Au labda, “katikati ya.”
Au “Funua uangavu wako.”
Tnn., “kuwaka hasira dhidi ya.”
Au “Shina kuu la mzabibu.”
Au “ulitazame tawi ambalo umelitia nguvu.”
Tnn., “kwa kemeo la uso wako.”