Zaburi 81:1-16

  • Wahimizwa watii

    • Msiabudu miungu ya kigeni (9)

    • ‘Laiti mngesikiliza’ (13)

Kwa kiongozi; juu ya Gitithi.* Wa Asafu.+ 81  Mshangilieni Mungu kwa sauti, nguvu zetu.+ Mpazieni sauti kwa ushindi Mungu wa Yakobo.   Anzisheni muziki na kuchukua tari,Kinubi chenye sauti tamu pamoja na kinanda.   Pigeni pembe wakati wa mwezi mpya,+Wakati wa mwezi mpevu, kwa ajili ya siku ya sherehe yetu.+   Kwa maana ni agizo kwa Israeli,Sheria ya Mungu wa Yakobo.+   Aliiweka ili iwe kikumbusho kwa Yosefu+Alipoenda* kuishambulia nchi ya Misri.+ Nilisikia sauti* ambayo sikuitambua:   “Niliuinua mzigo kutoka begani mwake;+Mikono yake iliwekwa huru kutoka kwenye kikapu.   Katika taabu uliita, nami nikakuokoa;+Nilikujibu kutoka katika wingu lenye ngurumo.*+ Nilikujaribu katika maji ya Meriba.*+ (Sela)   Sikieni, watu wangu, nami nitatoa ushahidi dhidi yenu. Ee Israeli, laiti ungenisikiliza.+   Hakutakuwa na mungu yeyote wa kigeni miongoni mwenu;Nanyi hamtamwinamia mungu wa kigeni.+ 10  Mimi, Yehova, ni Mungu wako,Niliyekutoa nchini Misri.+ Fungua wazi kinywa chako, nami nitakijaza.+ 11  Lakini watu wangu hawakuisikiliza sauti yangu;Israeli hakujitiisha kwangu.+ 12  Kwa hiyo nikawaacha wafuate mioyo yao mikaidi;Walitenda mambo waliyofikiri yanafaa.*+ 13  Laiti watu wangu wangenisikiliza,+Laiti Israeli angetembea katika njia zangu!+ 14  Ningewatiisha haraka maadui wao;Ningeugeuza mkono wangu dhidi ya wapinzani wao.+ 15  Wale wanaomchukia Yehova watajikunyata mbele zake,Na mwisho* wao utakuwa wa milele. 16  Lakini atakulisha* ngano bora kabisa*+Na kukushibisha kwa asali kutoka mwambani.”+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Yaani, Mungu.
Au “lugha.”
Tnn., “katika mahali palipofichika pa ngurumo.”
Maana yake “Kugombana.”
Tnn., “Walitembea katika mashauri yao.”
Tnn., “wakati.”
Tnn., “atamlisha,” yaani, watu wa Mungu.
Tnn., “mafuta ya ngano.”