Zaburi 82:1-8

  • Mwito wa kutekeleza hukumu ya haki

    • Mungu anahukumu miongoni mwa “miungu” (1)

    • “Mteteeni mtu wa hali ya chini” (3)

    • “Ninyi ni miungu” (6)

Muziki wa Asafu.+ 82  Mungu anachukua mahali pake katika kusanyiko la Mungu;+Anahukumu katikati ya miungu:*+   “Mtaendelea mpaka lini kuhukumu bila haki+Na kuwapendelea waovu?+ (Sela)   Mteteeni* mtu wa hali ya chini na yatima.+ Mtendeeni kwa haki mtu asiye na uwezo na maskini.+   Mwokoeni mtu wa hali ya chini na maskini;Waokoeni kutoka mkononi mwa mwovu.”   Hawajui wala hawaelewi;+Wanatembea huku na huku gizani;Misingi yote ya dunia inatikiswa.+   “Nimesema, ‘Ninyi ni miungu,*+Ninyi nyote ni wana wa Aliye Juu Zaidi.   Lakini mtakufa kama wanadamu wanavyokufa;+Nanyi mtaanguka kama mkuu mwingine yeyote anavyoanguka!’”+   Inuka, Ee Mungu, uihukumu dunia,+Kwa maana mataifa yote ni yako.

Maelezo ya Chini

Au “walio kama miungu.”
Au “Hukumuni kwa ajili ya.”
Au “ni kama miungu.”