Zaburi 83:1-18

  • Sala ya mtu anayekabili maadui

    • “Ee Mungu, usinyamaze” (1)

    • Maadui ni kama mwiba unaopeperushwa (13)

    • Jina la Mungu ni Yehova (18)

Wimbo. Muziki wa Asafu.+ 83  Ee Mungu, usinyamaze;+Usikae kimya wala kutulia, Ee Mungu.   Kwa maana, tazama! Maadui wako wanafanya fujo;+Wale wanaokuchukia wanatenda kwa kiburi.*   Kwa hila wanapanga njama kwa siri dhidi ya watu wako;Wanapanga njama dhidi ya watu wako unaowathamini.*   Wanasema: “Njooni, acheni tuwaangamize wakiwa taifa,+Ili jina la Israeli lisikumbukwe tena kamwe.”   Kwa umoja wanatunga mbinu;*Wameungana* dhidi yako+   Mahema ya Edomu na Waishmaeli, Moabu+ na Wahagri,+   Gebali na Amoni+ na Amaleki,Ufilisti+ pamoja na wakaaji wa Tiro.+   Pia Ashuru+ imejiunga nao;Wanawaunga mkono* wana wa Loti.+ (Sela)   Watendee kama ulivyoitendea Midiani,+Kama ulivyomtendea Sisera na Yabini kwenye kijito cha* Kishoni.+ 10  Waliangamizwa kule En-dori;+Wakawa mbolea juu ya ardhi. 11  Wafanye viongozi wao wawe kama Orebu na Zeebu+Na wakuu* wao kama Zeba na Zalmuna,+ 12  Kwa maana walisema: “Na tuimiliki nchi ambamo Mungu anakaa.” 13  Ee Mungu wangu, wafanye wawe kama mchongoma unaopeperushwa,*+Kama majani makavu yanayopeperushwa na upepo. 14  Kama moto unaoteketeza kabisa msitu,Kama mwali wa moto unaounguza milima,+ 15  Wafuatie vivyo hivyo kwa tufani yako+Na kuwaogopesha kwa dhoruba yako ya upepo.+ 16  Funika nyuso zao kwa aibu,*Ili walitafute jina lako, Ee Yehova. 17  Na waaibishwe na kuogopeshwa milele;Na wafedheheshwe na kuangamia; 18  Na watu wajue kwamba wewe, ambaye jina lako ni Yehova,+Wewe peke yako ndiye Uliye Juu Zaidi, juu ya dunia yote.+

Maelezo ya Chini

Au “wanainua vichwa vyao.”
Tnn., “waliofichwa.”
Tnn., “Wanashauriana kwa moyo mmoja.”
Au “Wamefanya agano.”
Tnn., “Wamekuwa mkono kwa.”
Au “korongo la.”
Au “viongozi.”
Au “kama mbaruti.”
Tnn., “Jaza nyuso zao aibu.”