Zaburi 84:1-12

  • Kutamani sana hema tukufu la Mungu la ibada

    • Mlawi atamani kuwa kama ndege (3)

    • “Siku moja katika nyua zako” (10)

    • “Mungu ni jua na ngao” (11)

Kwa kiongozi; juu ya Gitithi.* Muziki wa wana wa Kora.+ 84  Jinsi linavyovutia sana* hema lako tukufu la ibada,+Ee Yehova wa majeshi!   Nafsi yangu yote inatamani,Naam, ninazimia kwa kutamani,Nyua za Yehova.+ Moyo wangu na mwili wangu humshangilia kwa sauti Mungu aliye hai.   Hata ndege hupata makao hukoNa mbayuwayu hujipatia kiota,Ambamo huyatunza makinda wakeKaribu na madhabahu yako tukufu, Ee Yehova wa majeshi,Mfalme wangu na Mungu wangu!   Wenye furaha ni wale wanaokaa katika nyumba yako!+ Wanaendelea kukusifu.+ (Sela)   Wenye furaha ni watu wanaopata nguvu kutoka kwako,+Ambao mioyo yao inatamani sana* barabara kuu.   Wanapopita katika Bonde la Mibaka,*Wanalifanya kuwa mahali penye chemchemi;Na mvua ya mapema hulivisha* baraka.   Wataendelea kutembea kutoka nguvu hadi nguvu zaidi;+Kila mmoja wao hufika mbele za Mungu kule Sayuni.   Ee Yehova Mungu wa majeshi, isikie sala yangu;Sikiliza, Ee Mungu wa Yakobo. (Sela)   Tazama, ngao yetu+ na Mungu wetu,*Utazame uso wa mtiwa-mafuta wako.+ 10  Kwa maana siku moja katika nyua zako ni bora kuliko siku elfu moja kwingineko!+ Ninachagua kusimama kwenye kizingiti cha nyumba ya Mungu wanguBadala ya kukaa katika mahema ya uovu. 11  Kwa maana Yehova Mungu ni jua+ na ngao;+Yeye hutoa kibali na utukufu. Yehova hatawanyima jambo lolote jemaWale wanaotembea kwa utimilifu.+ 12  Ee Yehova wa majeshi,Mwenye furaha ni mtu anayekutumaini.+

Maelezo ya Chini

Angalia Kamusi.
Au “linavyopendwa sana.”
Tnn., “inakazia.”
Au “bonde lenye vichaka vya mibaka.”
Au labda, “Na mfundishaji hujifunika mwenyewe.”
Au labda, “Itazame ngao yetu, Ee Mungu.”